HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 2, 2017

WAZIRI MAGHEMBE AONGOZA MKUTANO WA SIKU YA WANAYAMAPORI NCHINI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Professa Jumanne Maghembe(wa pili kutoka kushoto) akizungumza na wafanyabiashara kwenye mkutano wa majadiliano kati ya Serikali na Sekta binafsi katika kulinda na kuhifadhi Maliasili hasa za wanyama pori kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar leo.(Picha na Karama Kenyunko wa Blogu ya Jamii)
Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi akizungumza na wafanyabiashara pamoja na viogozi juu ya uhifadhi wa wanayamapori leo kwenye ukumbi wa mkutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar. katika mkutano huo wafanyabiashara wameahidi kuipatia serikali uwezo zaidi  wa kupambana na ujangili dhidi ya wanyamapori.
Balozi wa Uhifadhi wanyamapori, Jacqueline Mengi akizungumza kuhusu uzuiaji wa ujangili kwa wanyamapori kwenye ukumbi wa mkutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar
 Baadhi ya wadau wakiwa kwenye mkutano wa majadiliano kati ya Serikali na Sekta binafsi katika kulinda na kuhifadhi Mali asili hasa za wanyamapori.
Waziri wa Maliasili na utalii, Prof. Jumanne Maghembe akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza mkutano wa majadiliano kati ya Serikali na Sekta binafsi katika kulinda na kuhifadhi Mali asili hasa za wanyama pori.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad