HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 1, 2017

TRA NA WASHAURI WA KODI 100 WAJADILIANA SHERIA ZA KODI

 Mkurugenzi wa Divisheni ya Mashauri ya Madai na Usuluhishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,  Obadia Kameya akifungua semina ya  elimu ya sheria za kodi iliyofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ambapo washauri wa masuala ya kodi walijadili namna ya utekelezaji wa mabadiliko mbalimbali katika sheria za kodi nchini.
 Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Richard Kayombo akizungumza wakati wa semina ya  kujadili namna bora ya utekelezaji wa mabadiliko katika sheria za kodi iliyofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania.
 Washauri wa masuala ya Kodi (Tax Consultants) walioshiriki katika semina ya kujadili namna bora ya utekelezaji wa mabadiliko ya sheria za kodi nchini iliyotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kushirikiana na kampuni ya ushauri wa masuala ya kodi ya Hanif Habib & Co.Semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Benki Kuu jijini dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Divisheni ya Mashauri ya Madai na Usuluhishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,  Obadia Kameya akiwa katika picha ya pamoja na Washauri wa masuala ya kodi (Tax Consultants) baada ya semina ya majadiliano ya namna bora ya utekelezaji wa mabadiliko na maboresho katika sheria za kodi nchini kuisha.Semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa benki kuu ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad