HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 1, 2017

OPERESHENI YA KUSAKA WASAMBAZAJI WA POMBE ZA VIROBA YAANZA RASMI LEO

 Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche akikagua moja ya pombe aina ya Kiroba Original mapema hii leo jijini Dar es Salaam wakati wa operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
 Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche (kulia) akipata maelekezo toka kwa msimamizi wa ghala lanalohifadhi pombe aina ya kiroba original Bw. Mhina Rashid (kushoto) Original mapema hii leo jijini Dar es Salaam wakati wa operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika, katikati ni Mkaguzi wa Chakula toka TFDA Bw. John Nzila.

Sehemu ya Shehena ya maboksi ya pombe aina ya Kiroba Original ilikutwa katika ghala lililopo  Mabibo jijini Dar es Salaam.
 Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche akizungumza na waandishi wa habari katika ghala la kuhifadhi pombe aina viroba  lililopo Mabibo jijini Dar es Salaam wakati wa operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
 Msimamizi wa Kiwanda cha Afro American Industries ambacho kinatengeneza pombe aina ya Viroba akitoa maelezo kwa Mwanasheria wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche wakati wa operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
 Mwanasheria toka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw. Manchare Heche akikagua baadhi ya nyara za Kiwanda cha Afro American Industries ambacho kinatengeneza pombe aina ya Viroba wakati wa operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.
Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira toka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Mayungi (Kushoto) akisisitiza jambo kwa Msimamizi wa Kiwanda cha Afro American Industries ambacho kinatengeneza pombe aina ya Viroba mapema hii leo jijini Dar es Salaam wakati wa operesheni ya kusaka wasambazaji wa kinywaji hicho ambacho Serikali imepiga marufuku kutumika.

Picha zote na Eliphace Marwa - Maelezo

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad