Katibu wa Umoja wa waandishi wa Riwaya wenye Dira(UWARIDI) Bw.Ibrahim Gama akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa programu(App) ya kuuza ,kununua na kusoma riwaya kwa njia ya simu iitwayo “UWARIDI APP” iliyozinduliwa na Umoja huo leo Jijini Dar es Salaam.Kulia kwake ni Rais wa UWARIDI Bw.Hussein Tuwa.
Rais wa Umoja wa waandishi wa Riwaya wenye Dira(UWARIDI) Bw.Hussein Tuwa akizungumzia uanzishwaji wa programu(App) ya kuuza ,kununua na kusoma riwaya kwa njia ya simu iitwayo “UWARIDI APP” iliyozinduliwa na Umoja huo leo Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Katibu wa Umoja wa umoja huo Bw.Ibrahim Gama na Abdillahi Muna kutoka Dau Technology ltd.
Mwakilishi kutoka Dau Technology Limited Bw.Abdillahi Muna(wa kwanza kulia) akieleza jinsi program ya “UWARIDI APP” iliyozinduliwa leo na Umoja wa waandishi wa Riwaya wenye Dira(UWARIDI) kwa ajili ya kuuza ,kununua na kusoma riwaya kwa njia ya simu.Dau Technology ndio watengenezaji wa App hiyo.Wengine ni Rais wa Umoja huo Bw.Hussein Tuwa na katibu wake Bw.Ibrahim Gama.
Viongozi wa Umoja wa waandishi wa Riwaya wenye Dira(UWARIDI)Rais wa umoja huo Bw.Hussein Tuwa na Katibu wake Bw.Ibrahim Gama wakionyesha waandishi wa nembo ya program yao mpya waliyoizindua leo Jijini Dar es Salaam.
Picha na Daudi
Manongi-MAELEZO.
Na Daudi Manongi-MAELEZO
Umoja wa waandishi wa Riwaya wenye Dira (UWARIDI)
umezindua mfumo maalum wa kuuza,kununua na kusoma riwaya kwa njia ya simu
iitwayo “UWARIDI APP” leo Jijini Dar es Salaam.
Akizindua Programu hiyo Katibu Mkuu wa Umoja huo
Bw. Bw.Ibrahim Gama amesema kuwa wameamua kuanzisha programu hii ili
kuwawezesha wanachama wa UWARIDI kuweka riwaya zao kwa ajili ya kuuzwa na wao
kujipatia malipo kutoka kwa mtengenezaji wa app hiyo.
“Kwa miaka mingi waandishi wa riwaya wamekuwa
wakijaribu kutafuta njia mbalimbali za kunadi kazi zao ili kuwafikia wasomaji
wao kwa urahisi,na tukaona changamoto wanazopata katika kuzipata kazi zetu na
hivyo tukaamua kuandaa program hii itakayowawezesha kupata riwaya zetu kwa
urahisi zaidi kwani utahitaji kuwa na programu hii tu kwenye simu yako ili
kusoma muda wowote”,Aliongeza Bw.Gama.
Katika mfumo huo kutapatikana riwaya za waandishi
mchanganyiko ikijumuisha waandishi nguli na wachanga ambapo mpaka sasa zaidi ya waandishi 20
wameweka riwaya zao katika mfumo huo na zinaendelea kuongezeka kila siku.
Aidha sababu kuu za kuanzisha mfumo huu ni wauzaji
wa vitabu vya riwaya wamekuwa hawapati malipo ya vitabu vyao kwa wakati wanapozikabidhi
kwa wachuuzi wa vitabu kwa utaratibu wa kupata malipo baada ya kuuza vitabu
hivyo, pia kukosekana kwa maduka rasmi ya vitabu vya riwaya nchini na wasanii
wachanga na wanaochipukia kutokuwa na
uwezo wa kifedha wa kuchapa vitabu.
Kwa upande wake Rais wa UWARIDI Bw.Hussein Tuwa alieleza
faida za mfumo huo kwa watumiaji wake kwa kusisitiza kuwa kazi zitakazokuwa
katika mfumo huo zitakuwa salama kwa kutoweza kunakiliwa na kuuzwa nje ya
mfumo,pia waandishi wake watapata pesa kwa wakati,waandishi wachanga ambao
hawajaweza kuchapisha vitabu vyao wataweza kuweka kazi zao kwa urahisi tofauti
na kusubiri kuzi kuchachapwa kitabuni pamoja na wasomaji walioko mbali na
maeneo walipo waandishi watazipata riwaya hizi kwa urahisi na wakati wowote.
UWARIDI ni umoja uliosajiliwa rasmi serikalini mwaka
2016 ukiwa unaundwa na mchanganyiko wa waandishi mahiri na wale wanaochipukia
katika uandishi wa riwaya nchini.
No comments:
Post a Comment