HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 28, 2017

NAPE AMKABIDHI RASMI OFISI WAZIRI MWAKYEMBE

 Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akiwakaribisha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison George Mwakyembe na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Nape Moses Nnauye kwa ajili ya makabidhiano rasmi ya Ofisi yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma.
  Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akitoa neno kwa Waziri mpya na Waziri aliyepita wakati wa makabidhiano rasmi ya Ofisi yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma.
 Mhe. Nape Moses Nnauye aliyekuwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo akitoa shukurani zake kwa watendaji wa Wizara kwa muda wote aliotumikia Wizara katika makabidhiano rasmi ya Ofisi yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison George Mwakyembe akimshukuru aliyekuwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye kwa kuitumikia Wizara kwa muda wote aliokuwepo.

 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison George Mwakyembe na aliyekuwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye wakitia saini hati za makabidhiano  rasmi ya Ofisi yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma akishubudia utiaji wa saini ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo  Prof Elisante Ole Gabriel.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison George Mwakyembe na aliyekuwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye wakikabidhiana hati za makabidhiano  rasmi ya Ofisi yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison George Mwakyembe na aliyekuwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri Mhe. Anastazia Wambura ,Katibu Mkuu wa Wizara hiyo  Prof Elisante Ole Gabriel, Naibu Katibu Mkuu Bibi Nuru Millao na watendaji wa Wizara mara baada ya mkabidhiano rasmi ya Ofisi yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma.

Picha zote na Raymond Mushumbusi WHUSM Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad