HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 2, 2017

TUNAPENDA JIJI LA DAR LIENDELEE KUNG'AA KWA USAFI, LAKINI SIO KWA MTINDO HUU

 ilianza kama masihara lakini sasa imekuwa ni kama mtindo mwendelezo wa kuhifadhi taka kando ya barabara, hivi inawezekanaje mtu anafanya usafi maeneo ya nyumbani kwake na kukushanya taka na kuja kuzibwaga kando ya barabara kama aonekanavyo mdau huyu?? inamaana hizi barabara ndio zinatakiwa kuwa chafu siku zote huku makwenu kukionekana kuko maridadi?? kwa taarifa yako, kuwezi kaa huko na kujisifia kuwa wewe ni mtunzaji mzuri wa mazingira na hodari wa usafi kwa kuja kubwaga taka katika maeneo kama haya. kwani usafi wa mji huanza na wewe kuanzia nyumbani kwako mpaka katika maeneo haya, na Dar es salaam safi inawezekana kabisa ikianza kwangu na kwako wewe hapo. ni hayo tu, hivyo tujipange vyema.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad