Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasaliano Mhe. Profesa Makame Mbarawa (katikati) akimsikiliza Mkuu wa Kivuko cha MV Kilambo kinachomilikiwa na TEMESA Jaston Mbawala wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya mkoani Mtwara. Kulia kwa Waziri ni Mhandisi Samwel Chibwana wa TEMESA Mtwara.
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mkoa wa Mtwara Mhandisi Saidi Mongomongo akimuelezea jambo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Profesa Makame Mbarawa alipotembelea kivuko cha MV Kilambo kilichopo mkoani Mtwara kinachotoa huduma mto Ruvuma mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Profesa Makame Mbarawa akikagua injini ya
kivuko cha MV Kilambo kinachotoa huduma mto Ruvuma kati ya Kilambo, Tanzania na
Namoto, Msumbiji. Picha
na Alfred Mgweno, TEMESA
Na Alfred Mgweno, TEMESA Mtwara.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Profesa Makame Mbarawa ametembelea na
kukagua kivuko cha MV Kilambo kilichopo Mkoani Mtwara mpakani mwa Tanzania na
Msumbiji. Kivuko hicho kinavusha magari, abiria na mizigo kati ya Kilambo
upande wa Tanzania na Namoto Msumbiji.
Akiwa
katika ziara hiyo Profesa Mbarawa aliambatana na viongozi mbalimbali wa Taasisi
zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano mkoani hapa. Profesa
Mbarawa alikaribishwa na Mkuu wa Kivuko
hicho Jaston Mbawala, Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wa Mkoa wa
Mtwara Mhandisi Saidi Mongomongo, Mhandisi
Msaidizi wa Kivuko Samwel Chibwana pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya
Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko Mhandisi Japhet Y. Maselle.
Akiwa
kivukoni hapo, Profesa Mbarawa alipata wasaa wa kusikiliza baadhi ya changamoto zinazokikumba kivuko hicho ambapo
Mhandisi Saidi Mongomongo alitaja changamoto hizo kuwa ni upungufu wa maji
nyakati za kiangazi, ubovu wa maegesho ambayo husababisha magari makubwa kunasa
wakati yanatoka au kuingia ndani ya kivuko pamoja na kukosekana kwa boti ndogo
za uokoaji ambazo zingesaidia wakati wa dharura.
Baadae
Profesa Mbarawa alipata fursa ya kuongea na watumishi walio chini ya Wizara
yake katika kikao kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa mkoa huku akiwataka watumishi
kuendelea kushirikiana na serikali, kufanya
kazi kwa kasi na uadilifu kwa kuzingatia weledi. Pia aliwataka watumishi kujenga
tabia ya kujitoa kwa ajili ya nchi yao.
Profesa
Mbarawa alikuwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo kwa nia ya
kutembelea na kukagua utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya wizara yake.
No comments:
Post a Comment