Na Greyson Mwase, Arusha
Imeelezwa
kuwa vyanzo vya nishati jadidifu kama vile upepo, jua, jotoardhi vitachangia
upatikanaji wa nishati ya uhakika ya umeme kwa kila kijiji ifikapo mwaka 2030 kama mpango wa
nishati kwa wote unavyofafanua.
Hayo
yameelezwa na Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na
Madini, Mhandisi Styden Rwebangila katika mafunzo kwa wadau wa nishati jadidifu kuhusu matumizi ya
mfumo mpya wa uhifadhi data na utoaji taarifa kwa ajili ya nishati jadidifu ujulikanao kama Tanzania Renewable Energy
Management Information System (TREMIS) yaliyofanyika jijini Arusha
leo
Mhandisi
Rwebangila alisema kuwa ili nchi ya Tanzania kuingia kwenye orodha ya nchi za
kipato cha kati ifikapo mwaka 2025, nishati ya uhakika ya umeme inahitajika
hususan katika kuchochea uwekezaji katika viwanda na kukuza uchumi wa nchi.
Alisema
mbali na gesi iliyogunduliwa katika mkoa wa Mtwara na maeneo mengine, nishati
ya umeme kutokana na vyanzo vingine kama vile upepo, jua, joto ardhi
vinahitajika ili kuongeza kiwango cha umeme katika Gridi ya Taifa.
“
Kuna maeneo ambayo hayajafikiwa na miradi mikubwa ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO) kama
visiwani, ambapo Wizara ya Nishati na Madini imeweka utaratibu wa kutumia
vyanzo vya nishati mbadala kama jua, upepo na jotoardhi kulingana na maeneo
husika ili kila mwananchi afikiwe na huduma ya umme,” alifafanua Mhandisi
Rwebangila.
Aliendelea
kusema kuwa ili kuvutia fursa za uwekezaji, Wizara imeanzisha mfumo mpya wa
uhifadhi data na utoaji taarifa kwa
ajili ya nishati jadidifu ujulikanao
kama Tanzania Renewable Energy
Management Information System (TREMIS) utakaowezesha wawekezaji
kutoka ndani na nje ya nchi kupata taarifa kuhusu fursa za uwekezaji katika
nishati jadidifu, sera na taratibu.
Alisema
kuwa taarifa za kampuni zote zinazojihusisha na nishati jadidifu, fursa za
uwekezaji, sera, sheria na taratibu zitawekwa katika mfumo huo utakaounganishwa
na tovuti ya Wizara ili wadau kupata uelewa kabla ya kuwekeza.
Aliendelea
kusema kuwa hatua iliyofikiwa kwa sasa
katika maandalizi ya mfumo huo, ni utoaji wa mafunzo na ukusanyaji wa maoni
kutoka kwa wadau mbalimbali wa nishati mbadala nchini ambapo mpaka sasa
wamekwishafanya zoezi hilo katika Kanda ya Ziwa.
Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi, Styden Rwebangila (kulia) akibadilishana mawazo na Mtaalam kutoka Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)- Wizara ya Nishati na Madini, Danford Phiri (kushoto) katika mafunzo yaliyokutanisha wadau wa nishati jadidifu jijini Arusha Februari 16, 2017
Wadau wa nishati jadidifu wakiendelea na majadiliano katika mafunzo hayo
No comments:
Post a Comment