HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 2, 2017

HALI YA MWANASOKA WA ZAMANI WA YANGA NA TAIFA STARS, GODFREY BONY NI MBAYA SANA, KALAZWA HOSPITALI YA MAKANDANA TUKUYU NA HAJITAMBU

Kiungo wa zamani wa timu ya Yanga, Tanzania Prisons na Taifa Stars, Godfrey Bony, amelazwa katika Hospitali ya Rungwe mkoani Mbeya huku akiwa hana fahamu.

Akizungumza na Mwandishi wetu Dada wa mchezaji huyo aliyejulikna kwa jina la Neema Boniface, alisema kuwa Bony alianza kuumwa ugonjwa usiojulikana miezi mitatu iliyopita na mpaka sasa bado haijajulikana anaumwa ugonjwa gani.

"Alikua anaumwa lakini alikua na nguvu zake, alikua anatoka anaenda kwenye shughuli zake, wakati mwingine anaenda kuangalia mpira" Alisema dada huyo.

Neema aliendelea kueleza kwamba wiki mbili zilizopita hali ya Bony, ilibadilika ghafla na kuwa mbaya zaidi ambapo alikua akilalamika kuishiwa nguvu na wakati mwingine kupoteza fahamu hali iliyolazimu kupelekwa hospitali.

"Tulimleta hospitali ya Makandana, Hospitali ya wilaya ya Rungwe lakini vipimo havikuonesha ugonjwa wowote ndiyo juzi ikabidi apigwe X Ray ya kifua na vipimo tumeambiwa vimetoka jana lakini jioni wakati madaktari wameishaondoka kwa hiyo wamesema watatupatia leo".

Kwa mujibu wa maelezo ya dada huyo ni kwamba hali ya kaka yake si nzuri kwa sababu hana fahamu.

Wadau wa Soka popote nchini, TFF na wapendasoka wote kwa ujumla mnaombwa kujitokeza kumsaidia Godfrey Bony ili aweze kupata matibabu husika na kujua ugonjwa unaomsumbua ili nyota huyu wa taifa aliyetoa jasho lake kuipeperusha bendera ya taifa letu aweze kupata msaada wa matibabu na hatimaye kurejea katika hali yake ya kawaida. 

Kwa yeyote mwenye nia njema ya kumsaidia Godfrey anaweza kuwasiliana na dada yake kwa simu namba 0765 359 290. Chanzo: mtandao wa wapenda soka

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad