HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, December 17, 2016

BWANAHARUSI ALALA MBELE NA KUMUACHA BI HARUSI KANISANI MUDA MCHACHE KABLA YA NDOA

Na JamiiMojaBlog, FahariNews

Mwisho wa mwaka 2016 huenda ukamaliza na kituko cha aina yake katika Mitaa ya Isanga Jijini Mbeya mara baada ya bwanaharusi kuingia mitini masaa machache kabla ya kufunga ndoa.

Tukio hilo la aina yake limeibua maswali mengi kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao walikuwa tayari kwa maandalizi ya kuhudhuria harusi hiyo kuanzia kanisani hadi ukumbini.

Imeelezwa kuwa mipango yote ya harusi ilifanyika kwa pande zote mbili kushiriki kwa kufuata taratibu zote zinazotakiwa kufuatwa hadi hatua ya mwisho ya kuingia kanisani ambapo kama kawaida ndugu na jamaa wote walihudhuria kanisani kwa lengo la kushuhudia tukio hilo .

Tukio rasmi lilianza majira ya saa 7 mchana katika kanisa la K.K.K.T Usharika wa Isanga jijini Mbeya Desemba 16 ambapo kama kawaida Bibi harusi akiongozana na wapambe wake akifuata na msafara wa magari zaidi ya manne akitokea Saloon na kuingia kanisani hapo.

Baada ya bibi harusi kuingia kanisani tayari kwa kufunga ndoa hiyo taarifa zilianza kuenea kuwa bwanaharusi hayupo kanisani hapo na hajulikani mahali alipo.

Kadri muda ulivyozidi kwenda bila bwana harusi kufika kanisani hapo baadhi ya Ndugu, jamaa na watu waliohudhuria harusi hiyo walianza kuhoji ambapo kwa muda huo yalipita zaidi ya masaa 4 bila chochote kuendelea kanisani hapo.

Akielezea mkasa huo Mchungaji kanisa la K.K.K.T Usharika wa Isanga Ndugu  Andagile Mwakijungu amesema jambo hilo amelipokea kwa masikitiko makubwa kwani halijawahi tokea toka ameanza kutoa  huduma kanisani hapo.

Amesema taratibu zote za kufungwa ndoa hiyo zilifanyika na Jana Desemba 15  majira ya saa 10 jioni  wahusika wote Samwel Mwakalobo   ambaye ni bwana harusi na Given Mgaya ambaye ni bibi harusi walifika nyumbani kwa baba mchungaji  na kuafikiana kuwa harusi hiyo ifanyike leo majira ya saa 7 mchana Desemba 16 kanisani hapo hivyo kitendo cha bwanahurusi kutofika bila sababu yoyote yeye mwenyewe imestua hasa kutokana na mipango ilivyokuwa imepangwa vizuri .

Amesema jambo hilo limetokea wakati yeye akiendelea kufanya maandalizi ya  kusubiri kutoa huduma ya kufunga ndoa kati ya wawili hao  .
 Gari lililombeba Bibi harusi likiwa limepaki nje ya Kanisa.

Amesema wakati akiendelea kusubiri ili kufungisha ndoa hiyo walitokea ndugu upande wa mume ambao waliomba msaada kwa mchungaji ili awasaidie kumtafuta kijana wao ambaye ni bwanaharusi  kwa njia yoyote ili kufaham chanzo kilichopelekea kushindwa kufika kanisani hapo bila kutoa sababu zozote.

Amesema alichukua jukumu la kumtafuta kijana huyo ambapo alifanikiwa kumpata na kuzungumza nae ambapo kijana huyo alimueleza kuwa anatatizo na baadae angefika   kwa mchungaji ili kumueleza.

“Baada ya wazazi kufika na kunieleza kuwa nisaidie kumtafuta kijana wao nilichukua jukumu hilo na nilifanya hivyo na nilifanikiwa kumpata lakini alicho nijibu nikuwa mchungaji ninatatizo hivyo nitafika ofisini kwako kukueleza na kwa sasa nipo njiani nikitokea Tunduma ”Amesema

Mchungaji amesema kuwa wakati wanaendelea na majadiliano ya nini kifanyike  ghafla walipata ujumbe kutoka kwa mpambe wa bwanaharusi ambao ulitumwa na bwanahaurusi mwenyewe ukieleza  kuwa asingeweza kufika ili kufunga ndoa hiyo bila kueleza sababu yoyote. 

Bibi harusi akitolewa kupitia mlango wa uwani wa kanisani huku akiwa amefunikwa khanga na wapambe wake kuelekea nyumbani baada ya shughuli ya ufungaji ndoa kushindikana kutokana na mume kuingia mitini pasipo sababu kufahamika katika kanisa la K.K.K T Usharika wa Isanga jijini Mbeya . 

Kufuatia tukio la bwanaharusi kuingia mitini huku jitihada za kumpata kushindiana Mchungaji huyo aliamua kusitisha zoezi la ufungaji wa ndoa hiyo.

“Nimejaribu kutafuta suluhisho la ndoa hii ili ifungwe licha ya kuchelewa lakini mpaka sasa hakuna dalili zozote kuwa ndoa hii itafungwa kwani bwanaharusi hajulikani alipo hivyo nimesitisha ndoa hii na niwaombee ndugu mkafanye jitihada zenu kumtafuta kijana huyu na mfikie muafaka kwa pande zote mbili ”Alisema Mchungaji.

 Amesema taratibu za ndoa zinataka siku 21 ndoa ifungwe hivyo yeye kama mchungaji kisheria ndiye mdhamini na mtangazaji wa kisheria kwa suala la ndoa ya mwaka 71 ambayo inampa mamlaka ya kueleza kwanini ndoa haikufungwa  kwa siku 21 kwa mujibu wa sheria.

Bibi harusi atolewa kanisani akiwa amevuliwa shera …………………

Katika kile ambacho kilisubiliwa kwa hamu na ndugu na jamaa kuona hitimisho la ndoa hiyo  ambapo bibi harusi aliingizwa katika gari maalumu bila kuvalishwa shera pamoja na kufunikwa kanga na kuondoka kanisani hapo majira ya saa 10 jioni wakielekea pasipo julikana huku baadhi ya ndugu wakionesha majonzi na wengine kutokwa na machozi kwa kutoa amni kile kilichotokea .

Waliochanga kwa ajili ya sherehe ya usiku……………

Mara baada ya sinema hiyo kukamilika kanisani ndugu na jamaa waliochanga pesa zao kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya usiku walianza kueleza kuwa watafika ukumbini kama kawaida na kula chakula na kunywa ili kufidia pesa yao.

Sherehe hiyo ilipangwa kufanyika katika Ukumbi wa Mkapa Hall jijini Mbeya na kuhudhuriwa na watu zaidi ya mia tatu ambapokila kwa michango wanakamati ilikuwa laki moja na wengine shilingi elfu 70.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad