HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 17, 2016

NIDA kuanza kutoa namba za utambulisho Desemba

Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imesema kuanzia Desemba mwaka huu mpaka Januari 2017 itaanza kutoa namba maalum za utambuzi kwa wananchi.

Mkakati huo umetangazwa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba alipokutana na uongozi na wafanyakazi wa NIDA, kwa lengo la kujadili mikakati mbalimbali ya kuboresha utendaji wa mamlaka hiyo.

Alisema tayari serikali imekamilisha kanzidata ya wananchi walizozipata kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC na kwamba, tayari taasisi zaidi ya 35 zimeanza kutumia taarifa za NIDA katika kufanya utambuzi wa wafanyakazi wao sawia na kupunguza usumbufu kwa wananchi kuhusu taarifa zinazowahusu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa NIDA Bw. Andrew Massawe alisema kwa zoezi la awali lililofanyika nchi nzima tayari wamefanya uhakiki wa kuwatambua watumishi wa serikali takribani laki tano na elfu sitini na tano.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad