HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 17, 2016

PROF. MBARAWA AHIMIZA SEKTA BINAFSI KUWEKEZA NCHINI

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akiteta na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Bi. Tonia Kandiero, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 10 wa Mashauriano wa wadau wa Sekta ya Uchukuzi, jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi), Dkt. Leonard Chamuriho akitoa hotuba wakati wa Ufunguzi wa mkutano wa 10 wa Mashauriano wa wadau wa Sekta ya Uchukuzi, jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga akitoa hotuba wakati wa Ufunguzi wa mkutano wa 10 wa Mashauriano wa wadau wa Sekta ya Uchukuzi, jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Bi.  Tonia Kandiero, akitoa hotuba wakati wa Ufunguzi wa mkutano wa 10 wa Mashauriano wa wadau wa Sekta ya Uchukuzi, jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akifungua mkutano wa 10 wa Mashauriano wa wadau wa Sekta ya Uchukuzi, jijini Dar es Salaam.
 Washiriki wa Mkutano wa 10 wa  Mashauriano  wa wadau wa Sekta ya Uchukuzi wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa  mkutano huo, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa maendeleo alipofungua mkutano Mkutano wa 10 wa  Mashauriano  wa Sekta ya Uchukuzi, jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amewataka wadau wa Sekta binafsi kujitokeza na kushirikiana na Serikali katika uwekezaji wa ujenzi wa miradi ya usafirishaji nchini.
Aidha amewataka wadau hao kuendelea kufadhili utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyo chini ya sekta hiyo ili kuchochea fursa za maendeleo.
Hayo ameyasema wakati akifungua mkutano wa 10 wa mashauriano wa wadau wa Sekta ya Uchukuzi na usafirishaji uliofanyika jijini Dar es Salaam.
“Michango ya Sekta binafsi inahitajika kwa kiasi kikubwa pamoja na Serikali kuendelea kutenga fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo”, amesema Prof. Mbarawa.
Prof. Mbarawa amesema kuwa mafanikio ya malengo ya mwaka jana ya mkutano huo yamepelekea Serikali kupitia sekta hiyo kuboresha usafiri wa anga kwa kununua ndege mbili za Bombadier Q400 mwaka huu.
Ameongeza kuwa kwa sasa Serikali ipo katika hatua za awali za ununuzi wa ndege nyingine tatu ambazo ndege ya kwanza itawasili Mwezi Julai mwakani na nyingine mbili zitawasili mwezi Mei na Septemba 2018.
“Mapitio ya mkutano wa 9 ni matunda ya upatikanaji wa ndege za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), hivyo mikutano kama hii ina tija kwani inaisaidia kuboresha hali ya miundombinu nchini”, amefafanua Waziri Prof. Mbarawa.
Amesisitiza wadau kutumia mkutano huo kama chachu ya kupata maoni na mawazo mapya ambayo yatasaidia katika kufanikisha uboreshaji wa Sera, Sheria  na kanuni za sekta ya usafarishaji nchini.
“Tumieni mkutano huu kujadili na kushauriana ili kupata majawabu yatakayosaidia kutatua changamoto zilizopo katika Sekta hii”, amesema Prof. Mbarawa.
Naye, Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Bi. Tonia Kandiero ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo katika uboreshaji na ukuzaji wa Sekta ya Usafirishaji ambayo ni kiungo kikubwa katika kukuza pato la Taifa.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Uchukuzi), Dr. Leonard Chamuriho amesema kuwa anaimani mkutano huo utasaidia kutatua changamoto za miradi mbalimbali iliyokuwa ikisuasua katika Sekta yake.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga amesema kuwa sekta yake imefanikiwa kuunganisha kwa kiwango cha lami barabara zote ndani ya mikoa na nchi jirani ambapo kwa sasa sehemu iliyobaki ni kuunganisha ukanda wa Magharibi.
Amezitaja barabara ambazo zipo katika ukanda huo kuwa ni Manyoni-Tabora-kigoma, Kigoma-Kidahwe-Kasulu, Kibondo-Nyakanazi, Sumbawanga-Mpanda-Uvinza-Kasulu, Tabora-Koga-Mpanda, Mbeya-Chunya-Makongorosi-Rungwe na Itigi mpaka Mkiwa.
Mkutano huo wa siku moja umewashirikisha wadau wa Sekta ya Uchukuzi na wafadhili mbalimbali katika kujadili miradi na utekelezaji wake pamoja na kutafuta suluhu za changamoto zinazoikabili sekta.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad