HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 17, 2016

GARI LA WIZI LAMPONZA PADRI WA KANISA KATOLIKI SUMBAWANGA

Kikosi Kazi cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam cha kuzuia wizi wa magari kimeendelea na kazi ya kudhibiti vitendo hivyo kwa kumkamata Padri wa Kanisa Katoliki Sumbawanga Demestrious Apolinary kwa tuhuma za kuhusika na ununuzi wa gari ya wizi.

Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro amesema mnamo Novemba, 11 baada ya padri huyo kununua gari aina ya Toyota L/cruiser T616 DCH mali ya Joseph Kayawaya lililoripotiwa kuibiwa Dar es Salaam na nyaraka za kughushi na kuuzwa jijini Arusha.

Amesema padri huyo anafanyiwa mahojiano na kwamba upelelezi utakapokamilika atapelekwa mahakamani ili kuona kama ni mnunuzi asiye na hatia au alishiriki kwa namna moja au nyingine katika wizi huo.

Kamanda Sirro amesema pia Jeshi la Polisi linashikilia watuhumiwa wengine wanne aliowataja kwa majina ya Aman Dickson, Exaud Martin, Rashid Haruna na Mzee Nasibu kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa magari katika matukio mawili tofauti.

Katika tukio lingine, Kamanda Sirro amesema Jeshi la Polisi linashikilia majambazi watano na vifaa mbalimbali walivyopora maeneo ya Tuwangoma mtaa wa Masaki, Mbagala.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad