HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, November 5, 2016

MSUVA MCHEZAJI BORA WA VPL MWEZI OKTOBA


WINGA Simon Msuva wa Young Africans amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Oktoba wa Ligi Kuu ya Vodacom.

Msuva alikuwa na washindani wa karibu wawili katika kinyang'anyiro hicho cha Oktoba ambao wote ni kutoka Simba. Wachezaji hao ni Shiza Kichuya na Mzamiru Yassin.

Katika mwezi Oktoba ambao ulikuwa na raundi sita, Msuva aliisaidia timu yake kupata jumla ya pointi 14 huku akifunga mabao manne, na kutoa pasi tano za mwisho (assist).

Kwa kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi, Msuva ambaye alikuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2014/2015 atazawadiwa kitita cha sh. milioni 
moja kutoka kwa wadhamini wa Ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad