HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, October 23, 2016

MSHIRIKI WA MISS TANZANIA, 2016 NO. 20 AIBUKA KIDEDE, CHEKI MPAMBANO WA MISS TALENT 2016 JINSI ULIVYOFANA.

Miss Talent 2016 ambaye ni Mshiriki wa Miss Tanzania 2016 namba 20 ameshika nafasi ya Kwanza katika mpambano wa Kusaka Vipaji kwa washiriki wa Miss Tanzania 2016 uliofanyika Jembe Beach jijini Mwanza leo. Mshindi huyo wa Miss Talent 2016 amecheza ngoma ya asili.
Mshindi wa Miss Talent 2016 akipongezwa na Mamiss wezake mara baada ya kushinda kinyang'anilo cha Miss Talent leo jijini Mwanza.
Top 5 Miss Talent 2016 wakiwa wamepozi mara baada ya kushinda nafasi tano Bora ya Miss Talent 2016.
Hashim Lundenga akitangaza Mshindi wa Kwanza wa Miss Talent 2015 mara baada ya Mamiss Tanzania Kufuana katika Kinyang'anyiro hicho na Miss Talent 2016 No. 20 kuibuka Kidedea.
 
Mshindi wa Pili wa Miss Talent 2016 akionesha Kipaji chake.
Mshindi wa tatu wa Miss Talent 2016 akifanya yake kwa kujifunga Mtandio kwa Mitindo mbalimbali.
Kulia ni Mshindi wa Nne namba 13 wa Mshindi wa Miss Talent 2016 akishirikiana na mwenzie kutumbuiza katika hafla ya kutafuta vipaji kwa mwamiss Tanzania 2016.
Mshindi wa Tano wa Miss Talent 2016 akisoma taarifa ya habari kwa Lugha ya Kiingereza na Kufananisha na watangazaji wa BBC World wakati wa kuonyesha kipaji chake jijini Mwanza Leo.



Mamiss Tanzania 2016 wakionesha Vipaji vyao wakicheza  katika hafla ya Kutafuta Miss Talent 2016 leo jijini Mwanza.
Vijana wakionesha umahili wao katika kucheza ngoma ya asili ya Kisukuma ijulikanayo  kama Zagamba leo katika hafla ya kutafuta Miss Talent 2016 jijini Mwanza.












Twist pale ikichezwa na Mshiriki wa Miss Tanzania 2016.






Washiriki wa Miss Tanzania 2016 wakionesha Vipaji vyao jijini Mwanza leo wakati wa Kusaka Mshindi wa Miss Talent 2016.


Pongezi.

Majiji wakifanya yao.
Baadhi ya watazamaji wakishuhudia Kinyang'anyiro cha Miss Talent 2016 jijini Mwanza leo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii Mwanza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad