HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 22, 2016

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA WA BIASHARA NA UWEKEZAJI BAINA YA TANZANIA NA MOROCCO

Wafanyabiashara wa Tanzania na Morocco wakimsikiliza  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akihutubia kwenye mkutano wa Kwanza wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Morocco utakaoainisha fursa za uwekezaji baina ya nchi hizo mbili uliofanyika kwenye Hotel ya Hyatt Regency.


Katika Hotuba yake ya ufunguzi wa Mkutano wa kwanza wa wafanyabiashara na Wawekezaji wa Tanzania na Morocco Makamu wa Rais aliainisha maeneo mbali mbali ambayo yanaweza kuwa fursa nzuri ya kuwekeza Tanzania.

Baadhi ya maeneo hayo ni Kilimo,Utalii, Nishati, Mafuta na Gesi, Viwanda,Sekta ya Huduma, na Sekta ya Madini

Mbali na kuainisha  baadhi ya fursa Makamu wa Rais aliwahakikishia uwepo wa amani na usalama na sheria mbalimbali zinazolinda haki za wawekezaji.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia kwenye mkutano wa kwanza wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Morocco utakaoainisha fursa za uwekezaji baina ya nchi hizo mbili uliofanyika kwenye Hotel ya Hyatt Regency.
 Rais wa  Chama cha Wafanyabiashara wa Morocco Bi.Miriem Bensalah-Chaqroun, akihutubia kwenye mkutano wa kwanza wa Biashara na Uwekezaji baina ya Tanzania na Morocco uliofanyika kwenye Hotel ya Hyatt Regency.
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akizungumza wakati wa mkutano wa kwanza uliowakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania na Morroco.
 Sehemu ya wafanyabiashara kutoka Morocco wakifuatilia kwa makini mkutano huo.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad