HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 13, 2016

KIJANA WA KITANZANIA AHOFIWA KUFA MAJI NCHINI MAREKANI

KIJANA wa kitanzania Samson Charles Bidan (20) ahofiwa kupoteza maisha baada ya kufukiwa na mchanga uliokuwa unachimbwa baada ya mwaka 2011 kutokea kwa mafuriko nchini Marekani  na kuamua kuchimba ili kuruhusu maji yaende kwa urahisi. 

Bidani mwenye urefu wa futi saba  akiwa na rafiki zake katika  eneo la Kayaking walifika karibu na eneo la uvunjwaji wa shimo hilo la mchanga ikiwa inakadiriwa kuwa na urefu wa mita 50 hadi 80 kwenda chini na kufukiwa huku wenzie wakiokolewa na yeye mwili wake ukiwa haujapatikana mpaka muda huu.

Ajali hiyo imetokea Jumatatu usiku,  Sheriff Jerome Kramer amesema mwili wa Bidan bado haujapatikana  kwani kuna kiasi kikubwa cha mchanga katika eneo hilo na wanahisi kuwa kwamba uwezekano mkubwa wa kuwa kafunikwa na mchanga. 

Wafanyakazi wa eneo hilo wametumia muda mwingi kuzuia uvunjaji wakiwa na matumaini ya kuacha mtiririko ili kupunguza kiasi cha uchafu katika maji. Wakati huo huo, boti  mbalimbali zinaendelea kutafuta mwili wa  Bidan. Kramer anasema wao wanatambua eneo ambako alikwenda ndani ya maji, hivyo wanaendelea kutafuta eneo hilo sana.

Kitengo cha utelekezaji wa Sheria chini ya  Lincoln County Dive  na Nebraska Game wa Tume ya Hifadhi wote wamefanya juhudi za kuufikia mwili wa Bidan lakini bado hawajafanikiwa na kumeonekana kuwa na uchafu mwingi sana katika shimo hilo linalosadikiwa kuwepo kwa mwili huo na mpaka muda huu wameshindwa kupata picha nzuri chini ya uso wa maji.

Bidan, ni moja ya wacheza mpira wa kikapu nchini humo na tayari alikuwa amepangwa na Kocha wake Kevin O'Connor  katika timu ya chuo cha North Platte Community.  Dk Jody Tomanek, Makamu wa Rais wa North Platte Community College, alisema, "Hii ni ya kusikitisha na kutisha sana, ni pigo kubwa tumelipata kama chuo, Katika muda mfupi Samson alikuwa pamoja na wenzake Chuoni na amekuwa kivutio kwa wanafunzi  na wafanyakazi."

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad