HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 23, 2013

waimbaji nyota wa kimataifa wa muziki wa injili kutoka Afrika kusini na Rwanda kuwasili leo jijini dar tayari kwa tamasha la krismass

MKurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions Ltd,inayoandaa tamasha la Krismasi,Bwa.Alex Msama akizungumza na baadhi ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye viwanja vya Karimjee,jijini Dar jana wakati alipokuwa akielezea maandalizi ya lala salama ya tamasha hilo,linalotarajiwa kufanyika siku ya sikukuu ya Krisimasi,kwenye Uwanja wa Taifa.

Tamasha hilo litakalojumisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za kiroho wa hapa nyumbani sambamba na kutoka nje ya nchi ikiwemo nchini Afrika Kusini na Rwanda.Mwimbaji mahiri wa nyimbo za kiroho kutoka nchini Afrika Kusini,Solly Mahlangu na Liliani Kabaganza kutoka nchini Ruanda wanatarajiwa kuwasili jijini Dar leo tayari kwa ushiri wa tamasha hilo linalowakutanisha watazamaji lukuki.


Msama aliwataja baadhi ya Waimbaji watakatumbuiza kwenye tamasha hilo la Krisimas,kuwa ni Rose Muhando,Solomon Mukubwa,Upendo Nkone,Upendo Kilahiro,Anastazia Mukabwa,John Lissu,Boni Mwaitege,Ephrahim Sekeleti,Glorious Warship Team,The Voice Acapella,New Life Band na wengineo kibao.

Msama alisema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yamekwishakamilika na kinachosubiriwa mashambulizi tu yatakayoanzia jijini Dar,Morogoro,Tanga,Arusha na kumalizia mkoani Dodoma

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad