HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 23, 2013

matembezi ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Kikundi cha Brass Band cha Umoja wa Vijana CCM Zanzibar,kikiongoza matembezi ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar,yaliyofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,leo kuanzia Micheweni kuelekea Wete Mkoa wa Kasakazini Pemba.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,(wa pili kushoto)akiongoza Maandamano ua Umoja wa Vijana CCM Zanzibar yaliyoanzia Michweni kelekea Wete Pemba,leo katika ufunguzi rasmi,Makamo wa Rais wa Zanzibar na Mjumbe wa kamati Kuu Balozi Seif Ali Iddi,(kushoto) Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Sadifa Juma Khamis,(katikati) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai,na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa NEC Dk.Mauwa Daftari.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,alipokuwa akizungumza na Umoja wa Vijana wa CCM Zanzibar na Wanachama wa CCM Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba leo,pamoja na kuyafungua Matembezi ya Umoja huo ya Maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar, katika uwanja wa Mpira Micheweni kwa Shaamemata, (kushoto) Naibu Katibu Mkuu  wa CCM Zanzibar  Vuai Ali Vuai.
Vijana wa CCM Zanzibar,UVCCM wakiwa katika Matembezi ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,yaliyofunguliwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,(hayupo pichani)yaliyoanzia Micheweni kuelekea Wete Mkoa wa Kasakazini Pemba
 Vijana wa UVCCM wakiwa wamebeba Pich za Viongozi wa Chama katika Matembezi ya Madhimisho ya miaka 5o ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliyofunguliwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,(hayupo pichani)kuanzia Micheweni kuelekea Wete Mkoa wa Kasakazini Pemba. Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad