Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es salaam leo wakati wa kutangaza Jopo la wataalamu 20 aliowateua kwa ajili ya kupanga mkakati wa kuonesha jinsi Tanzania inavyoweza kushiriki Fainali za Afrika (AFCON) zitakazofanyika mwaka 2015 nchini Morocco. Jopo hilo la wataalam litakutana kwa siku tatu mjini Zanzibar kuanzia Desemba 6-8 mwaka huu. Jopo hilo litaongozwa na Mwenyekiti wa zamani wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Kanali mstaafu Idd Omari Kipingu.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Lager,George Kavishe akizungumza machache juu ya Kamati hiyo maalum,ambapo ameiombea mafanikio makubwa ili tuweze kuja kupata timu bora ya Taifa kwa siku zijazo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Jopo la wataalamu 20 watakaokutana Visiwani Zanzibar hivi karibuni,Kanali mstaafu Idd Omari Kipingu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo.
Mmoja wa Waandishi wa habari kutoka Chombo cha EATV,Patrick Nyembela akiuliza swali kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi (hayupo pichani).
No comments:
Post a Comment