Rais wa Zanbzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein,(katikati) akifuatana na Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao, wakielekea katika Mazishi ya Padri Evaristus Gabriel Mushi,aliyezikwa katika viwanja vya kanisa la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja
|
Vijana waumini wa Dini ya Kikiristo wakiteremsha jeneza lenye mwili wa marehemu Padri Evaristus Gabriel Mushi,katika kaburi alilozikwa leo katika viwanja vya kanisa la Katoliki la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja,marehemu alifariki kwa kupigwa risasi Jumapili iliyopita na watu wasiojulikanwa
|
Rais wa Zanbzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein,(katikati) akitia udongo katika kaburi la Marehemu Padri Evaristus Gabriel Mushi,wakati wa mazishi yake yaliyofanyika leo katika viwanja vya kanisa la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja
|
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Emanuel Nchimbi ,akitia udongo katika kaburi la Marehemu Padri Evaristus Gabriel Mushi,wakati wa mazishi yake yaliyofanyika leo katika viwanja vya kanisa la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja
|
ASkofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Muadhama Policup Kadinari Pengo,kwa pamoja na maaskofu wengine wakichomeka Msalaba katika kaburi la marehemu Padri Evaristus Gabriel Mushi,aliyezikwa leo katika viwanja vya kanisa Katoliki la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja,ambae alifariki Jumapili Iliyopita
kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana |
Rais wa Zanbzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein,(katikati) akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Padri Evaristus Gabriel Mushi,wakati wa mazishi yake yaliyofanyika leo katika viwanja vya kanisa la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
|
Baadhi ya waumini wa kanisa katoliki wakiwa katika mazishi ya marehemu Padri Evaristus Gabriel Mushi,aliyezikwa leo katika viwanja vya kanisa Katoliki la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja,
Picha na Ramadhan Othman,IKULU.
Na Maelezo Zanzibar
Mamia
ya Wananchi wa Zanzibar leo wameshiriki Mazishi ya Padri Evaristus
Mushi aliyeuwa kwa kupigwa Risasi na Watu wasiojulikana ambayo
yamefanyika katika kijiji cha Kitope Wilaya ya Kaskazini B,Unguja. Katika
mazishi hayo Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamo wa Kwanza
wa Rais Maalim Seif Shariff Hamad,Viongozi wa Serikali na Vyama vya
siasa walihudhuria.
Akitoa
salamu za Serikali katika Mazishi hayo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo
wa Pili wa Rais Mohammed Aboud Mohammed alisema Serikali imeguswa sana
na kifo cha Padri huyo na kuongeza kuwa itahakikisha waliohusika na
tukio la mauji hayo wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Kwa
upande wake Askofu wa Kanisa la Anglikacana Michael hafidh amewataka
Waamini wa dini ya kikristo kuwa watulivu bila kulipiza kisasi bali
waiachie Serikali kufanya kazi yake ili kuwabaini waliopoteza Uhai wa
Marehemu huyo.
Awali
Mazishi hayo yalitanguliwa na Misa takatifu ya kumuombea Marehemu
iliyoendeshwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es
Salaam Muadhama Policarp Kadinali Pengo katika Kanisa la Minara Miwili
Mjini Zanzibar.
Padri
Mushi alifariki dunia Februari 17 baada ya kupigwa risasi na watu
wasiojulikana wakati akielekea Kanisani kuendesha Misa ya Asubuhi katika
Kigangwe cha Mtakatifu Teresia eneo la Beit El Raas mjini Unguja Enzi
za uhai wake Padri Mushi alikuwa Msomi wa Shahada ya Uzamivu ya Elimu ya
Ushauri nasaha aliyoipata nchini Marekani ambapo umauti ulimkuta akiwa
anaelekea kuendesha Ibada ya Jumapili ya kwanza ya Kwarezma.
Padri
Evarist Mushi wa Kanisa la Minara Miwili mjini Zanzibar alizaliwa June
15, 1957 Mkoa wa Kilimanjaro akiwa ni mtoto wa nne katika familia ya
watoto sita ya Mzee Mushi.
No comments:
Post a Comment