Mkurugenzi Msaidizi wa Michezo katika Wizara ya Habari, Vijana, Michezo na Utamaduni, Juliana Yasoda (kulia) akimkabidhi tiketi ya ndege kwa mmoja wa wanariadha Shamba Gutine wanaokwenda kuiwakislisha nchi katika mashindano ya kimataifa ya riadha nchini Mali ( Bamako International Marathon) mashindano yanayotarajiwa kuanza kesho, wengine katika picha ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Afrika Tanzania Ammishi Owusu – Amoah (kulia) katikati ni Mkuu wa shughuli za kibiashara za Kibenki Wasia Mushi, mwisho kulia ni Mkuu wa Huduma za wateja wa Rejareja Mwanahiba Mzee.Tiketi hizo zimetolewa na benki hiyo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Michezo katika Wizara ya Habari, Vijana, Michezo na Utamaduni Juliana Yasoda (kulia) akimkabidhi bendera ya Taifa mmoja wa wanariadha Shamba Gutine wanaokwenda kuiwakislisha nchi katika mashindano ya kimataifa ya riadha nchini Mali ( Bamako International Marathon) mashindano yanayotarajiwa kuanza tarehe 13 januari mwaka huu, wengine katika picha ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Afrika Tanzania Ammishi Owusu – Amoah (kulia) katikati ni Mkuu wa Shughuli za Kibiashara za Kibenki Wasia Mushi, mwisho kushoto ni kocha wa wanariadha hao Shabani Hiki.Benki ya Afrika Tanzania imegharimia tiketi na pesa za kujikimu kwa wawakilishi hao.
No comments:
Post a Comment