HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 10, 2012

Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2012 wapata baraka za Mh. Lowassa mjini Monduli leo


 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimia na Miss Tanzania 2011,Salha Israel alieambatana na timu nzima ya Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2012 kwenye ziara ya kutembelea mikoa ya Kanda ya Kaskazini,wakati waliofika Nyumbani kwa Waziri Mkuu Mstaafu,Monduli leo kumsalimia na kupata baraka zake kwenye mashindano hayo.Kuli ni Mkurugenzi wa Rino Agency na Muandaaji wa Miss Tanzania,Hashim Lundenga na wa pili kushoto ni Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu,Mama Regina Lowassa.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimia na Msimamizi (Matron) wa warembo wa Redd's Miss Tanzania 2012,Irene Karugaba wakati Warembo hao walipotembelea Nyumbani kwa Waziri Mkuu Mstaafu,Monduli ili Kupata Baraka zake.Mh. Lowassa aliwapokea warembo hao kwa furaha na kuzungumza nao machache juu ya mafanikio ya Mashindano hayo na kuwapa hamasa ya kutokata tamaa hata mara moja.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimia na Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2012 waliofika Nyumbani kwake Monduli leo ili Kupata Baraka zake wakati wakijiandaa kuelekea kwenye fainali za Shindano hilo zitakazofanyika Novemba 3,2012 kwenye ukumbi wa Blue Peal,Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.Warembo hao wamekutana na Mh. Lowassa wakati wakiwa kwenye ziara ya kutembelea Mikao ya Kaskazini na kujifunza mambo mbali mbali ya Utalii wa ndani.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwapa somo Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2012 waliofika Nyumbani kwake Monduli leo.Kushoto ni Mke wake,Mama Regina Lowassa,Mkurugenzi wa Rino Agency na Muandaaji wa Miss Tanzania,Hashim Lundenga pamoja na Miss Tanzania wa Sasa,Salha Israel.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiendelea kuzungumza na Warembo hao.
Warembo wakimsikiliza kwa makini Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Mkurugenzi wa Rino Agency na Muandaaji wa Miss Tanzania,Hashim Lundenga akifafanua jambo kwa Mh. Lowassa na Mama Regina Lowassa.
Warembo wa Redd's Miss Tanzania wakiwa wamevalia mavazi ya Kimasai.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina Lowassa wakiwa kwenye picha ya pamoja na Warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Tanzania 2012 pamoja na Viongozi wa Kamati ya Miss Tanzania. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad