HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, January 8, 2012

Muwindaji Hachagui Pori ............. Mtu Mzima Mawindoni leo

 Naingia zangu Mawindoni huku Manati yangu Shingoni yakining'inia.
 Mtu Mzima nikimlia taimingi Cholwe
 Aahhh.... si alidondokea hapa,sasa kaenda wapi tena?? au ndio mambo ya nanihii yafanya kazi huku porini.
 Hapa nikiachia simkosi,haki ya nani tena vile.
Daahh... Kweli kisicho rizki hakiliki,yaani nimemkosa mara mbili zote...!!!,ngoja niongeze mawe nijaribu tena bahati yangu.

7 comments:

  1. mh staili nyingine za kuchimba dawa kiboko. Unajifanya unawinda kumbe unachafua pori letu huko Bagamoyo.

    ReplyDelete
  2. Hahahahhaahaha kakaaaa yaani leo nimecheka sana,yaani umenikumbusha mbali sana tuu,ok ukipata TETELE NAMI USINIKOSE!!!!!Angalia usiwindwe wewe tuu.

    ReplyDelete
  3. MSHIKAJI ACHA HAYO MAMBO YA KUFUNDISHA JAMII, KUUA NDEGE KWA MANATI. SIO POA HIO! KILA KIUMBE DUNIANI KINA STAHILI HAKI YA KUISHI BILA KUNYANYASWA . KWA NINI UWAWINDE HAO NDEGE WAMAKOSA NINI KAMA UNAHAMU YA NDEGE, KUKU WAPO WENGI TU TENA BEI POA. DUUU MJAMAA LEO NAONA KIDOGO UMENIBOA.

    HIO SIO MTAA KWA MTAA TENA LEO NAONA UMECHEMSHA TUTAACHA KUANGALIA BLOG YAKO KAMA HUTOJIREKEBISHA WEWE MPIGANAJI WA MAZINGIRA MBONA UNA AANZA YACHAFUA MWENYEWE?

    MDAU COPENHAGEN,DENMARK

    ReplyDelete
  4. Yaani mbavu zinavyoniuma ..nimekumbuka wakati nilipkuwa mdogodogo kaka zangu walikuwa wanapenda sana kuwinda ndege kwa manati..Kama Da Rachel hapa juu alivyosema angalia usiwindwe au haya manati yakakurudi:-) Inapendeza siku moja moja kukukumbuka michezo tuliyocheza tulipokuwa wadogo. ukipata usininyime:-)

    ReplyDelete
  5. Acha uchu kaka, kindege ukikipiga manati ndio ukalie ugali au? Kama unataka kuwinda chukua bunduki nenda porini....

    ReplyDelete
  6. hapa sio ulikuwa watafuta pori la kuchimba dawa? Acha kutuvunga kijana.

    ReplyDelete
  7. Mdau sioni kama Amekosea Toka uishi DENMARK ishakuwa tabu, yeye kaona sawa NDege kuliwa na kutunguliwa na manati kama huko kwenu Europe wanavyowapiga kwa Bunduki Ndege, ukisema ndege asiliwe ale kuku basi kaa juwa kuna nchi zengine nazo hawapendi huyo kuku aliwe na wala asichinjwe na kisu. ukisema sababu kina roho kaa juwa hata mimea ina roho usile majani pia.

    ReplyDelete

Post Bottom Ad