HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 4, 2011

FILAMU YA CHUMO YAPOKELEWA VYEMA NA JAMII JIJINI DAR

Wakazi wa jiji la Dar wakiwa wamefurika kwa wingi katika viwanja vya Biafra,Kinondoni jioni ya leo kushuhudia uzinduzi wa Filamu ya Kiswahili inayoitwa CHUMO ambayo inaelezea athari za ugonjwa wa Malaria wa wanawake wajawazito,iliyotengenezwa na Media For Development International - Tanzania chini ya Uongozi wa Jordan Riber.
Wakazi wa Maeneo mbali mbali ya jiji la Dar wakiangalia uzinduzi wa Filamu ya CHUMO katika viwanja vya Biafra,Kinondoni jioni ya leo.
Askari Polisi wakijaribu kuwapanga watu katika utaratibu uliowekwa ili kila mmoja aweze kuona Filamu hiyo.
Pamoja na kwamba kulikuwa na Manyunyu ya mvua ya hapa na pale lakini hakuna alietaka kuondoka eneo hilo la Biafra bila kuitazama Filamu hiyo ambayo ni nzuri na yakusisimua na pia inatoa mafunzo katika jamii kwa swala zima la kupiga vita ugonjwa wa Malaria hasa kwa kila mama wajawazito.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad