HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, August 22, 2010

wachezaji wasioitwa timu ya taifa,watakiwa kutokata tamaa - kocha paulsen

Kocha mkuu wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Jean Paulsen (kati) akiongea na waandishi wa habari mkoani Arusha (hawapo pichani) wakati alipokuwa akitangaza kikosi kipya cha timu hiyo kitakachokwenda nchini Algeria kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya Algeria hapo Septemba 4,mwaka huu.kulia ni Afisa Habari wa TFF, Florian Kaijage na kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Arusha ambaye pia ni mjumbe wa TFF,Alfa Mgonja wakimsikiliza kwa makini kocha huyo.


Na Woinde Shizza,Arusha

KOCHA wa timu ya Taifa (Taifa Stars) ,Jean Paulsen amezitaka timu zinashiriki katika ligi kuu ambazo wachezaji wake hawakubahatika kuchaguliwa katika kikosi cha timu ya Taifa kuwafanya wachezaji wao waweze kujituma na kujitahidi zaidi haswa katika kipindi hiki cha ligi kuu ili waweze kuonekana na kuchaguliwa.

Kocha huyo aliyasema hayo wakati alipokuwa akitangaza kikosi cha timu ya Taifa ambacho kinataraji kwenda nchini Algeria kushiriki mechi ya kirafiki dhidi ya timu hiyo ya Algeria ambayo inatarajiwa kuchezwa September 4 mwaka huu..

Alisema kuwa amechagua wachezaji hao kutokana na sifa za timu zao pamoja na viwango ambavyo ameviona kutoka kwa wachezaji hao katika mechi zao chache ambazo wamezicheza.

Alibainisha kuwa wachezaji kwa ujumla wanatakiwa wafuate sheria ambazo wanafundishwa na waalimu wao pamoja na kuzingatia sheria za mpira na kuzingatia mazoezi sana.

Alisema kuwa bado hajamaliza kuchagua kikosi cha timu ya taifa kwani ataendelea kuchagua kutokana na mechi ambazo ataziudhuria na kuziangalia na ataangalia viwango vya wachezaji pamoja na timu ambazo wanatoka na zinavyoongoza.

“mimi nimechagua wachezaji kulingana na timu zao pamoja na ubora wa mchezaji mwenyewe pamoja na uwezo wake wa kucheza mpira,napenda kuwasihi ambao sijawachagua kuwa wanatakiwa wajitahidi sana na wakionyesha ubora nitawachagua wala wasiwe na wasiwasi’’alisema Paulsen

Katika timu hii ambayo kikosi chake kimetajwa rasmi, kinajumla ya wachezaji 26 ambao na katika kikosi hiki kuna baadhi ambao watachujwa na pia katika kikosi hiki hakina tofauti sana na kikosi kilichopita.

Kocha mkuu wa timu hii ya taifa alisema kuwa katika kikosi chake hakumteuwa Kiggy Makasi pamoja ya kuwa alikuwa anauwezo wa kucheza kutokana na sababu za kiafya ambazo zinamsumbua mchezaji huyu.

Kikosi hiki cha timu ya Taifa kinatarajiwa kuondoka Agosti 31 kuelekea katika mechi yao ya kirafiki baina yao na timu ya nchini Algeria.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad