
Beki wa timu ya Taifa (Taifa Stars) Kelvin Yondan (kulia) akichuna vikali kuwania mpira na mshambuliaji wa Harambee Stars, John Barasa, wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru.mpaka mpira unamalizika matokeo yalikuwa ni Taifa Stars 1-1 Harambee

Kipa wa Taifa Stars, Shaban Kado, akiokoa hatari langoni mwake baada ya kupigwa kwa shuti kali na Dennis Oliech wa Harambee Stars wakati wa mchezo huo.

Wachezaji wa Taifa Stars, wakimpongeza Mrisho Ngassa, baada ya kuipatia timu yake bao la kusawazisha katika kipindi cha pili cha mchezo baada ya kumtoka beki na kumchungulia Kipa wa Harambee Stars Wilson Obungu aliyejaribu kutokea ili kuokoa na kupishana na mpira na kufanya matokeo kuwa 1-1.

Mariga akikosa bao na kuanguka langoni mwa Stars.
(Picha Zote kwa hisani Ya
Muhidin Sufiani Blog)
No comments:
Post a Comment