HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, January 15, 2010

Hoja Ya Mdau Joseph Kwa Elimu Ya Bongo

Yametolewa mapendekezo mengi kuhusu mikakati ambayo inapaswa kutumika ili kuboresha elimu yetu.

Pamoja na hiyo mikakati napendekeza Watanzania mahala tulipo tufanye jambo
hili:

Tujiunge pamoja kama watu watano mpaka 10 na kuchagua shule angalau moja ya msingi au sekondari na kupanga utaratibu wa kuitembelea angalau mara moja kila mwezi ili kuwahamasisha walimu na wanafunzi na kuona nini
kinaweza kufanyika kuiboresha shule husika.

Mpaka Julai mwaka jana 2009 idadi ya shule za msingi za Serikali ni 15301
kati ya shule 15727 za msingi hapa nchini.
Kwa upande wa sekondari idadi ya shule zote ni 4102. Kati ya hizo za
serikali ni 3283.

Kwa takwimu hizi idadi ya shule zetu ni chini ya elfu 20,000 wakati idadi
yetu kama Watanzania ni zaidi ya milioni 42.

Tuamue na kutenda na lazima tutaona mabadiliko chanya.

Salaam,
Josephat (Mfugaji)

kutoka
www.wanabidii.net

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad