HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 11, 2008

Waliokufa Katika Ajari Ya Helikopta

Huzuni ilitawala jana (Jumanne) wakati Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Isidori Shirima alipoongoza mamia ya watu katika kuaga miili ya watu sita waliokufa katika ajali ya Helikopya ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania iliyotokea mwishoni mwa wiki mkoani Arusha.
Katika ajali hiyo waliofariki dunia wamejulikana kuwa ni Kanali Wakete ambaye alikuwa rubani, Meja Sinda ambaye pia alikuwa rubani, Luten Kirunga ambaye alikuwa fundi,PTE Mambe(fundi),mke wa Brigedia Jitenga,Irene jitenga na mtoto wa Kanali Mzirai ambaye jina lake halikufahamika mara moja na ni mkazi wa Arusha.Habari na Joseph Ngilisho/Global Publishers Arusha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad