Bandari ya Kilwa iliyopo Kilwa Masoko Mkoani Lindi, imeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa Watalii kutoka Mataifa mbalimbali ambao wanaendelea kuwasili Nchini kujionea vituo vya Utalii.
Meli ya Watalii ya BOUGAINVILLE ambayo ni Meli ya tano kutia nanga Bandarini hapo, imewasili ikiwa na Watalii 133.
Tangu kuanza kuwasili kwa Meli hizo, jumla ya Watalii 593 Wametembelea Vivutio vya Utalii kwa mafanikio na kusifu huduma za Meli zinazotolewa na Wataalamu Wazawa wa TPA ambao wameonesha Weledi na umahiri mkubwa katika majukumu yao ya kuhudumia Meli hizo za Watalii.






No comments:
Post a Comment