Na Mwandishi wetu
Shirika Lisilo la Kiserikali (NGO) ,Thamani Women Tanzania, imezindua
kampeni yake ya kwanza ijulikanayo kwa kauli mbiu ya "Piga Mpira Sio
Mwanamke" yenye lengo la kukemea na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake
na watoto nchini Tanzania.
Uzinduzi huo umefanyika katika hotel
ya Hyatt,Regency kwa kushirikiana na timu za Ligi Kuu yaTanzania Bara,
Simba SC, Azam FC na Singida Fountain Gate na kuzinduliwa Naibu Waziri
wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Khamis Mwinjuma (FA).
Akizungumza
katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Thamani Women Tanzania, Nafue
NyangeE alisema kuwa taasisi hiyo iliamua kutumia mpira wa miguu kwa
lengo la kufikisha haraka na kwa kishindo ujumbe wao kwani mashabiki wa
mpira wa miguu kwa idadi kubwa Zaidi ni wanaume wa makamu na matabaka
tofauti.
Nyange alisema kuwa wachezaji wa timu hizo ambao
watarekodi sauti na video za kupinga vitendo kikatili na kusambazwa
katika mitandao ya kijamii, redio na wanaamini kuwa jamii itafikiwa kwa
haraka na kukomesha kabisa janga hili.
“Wanamichezo wana fadhila
na majukumu kwa mashabiki wao. Hakuna michezo bila mashabiki...lakini
pia hakuna mashabiki bila amani na upendo katika jamii. Mashabiki tuna
waazima wana michezo sauti zetu kwa shauku kubwa katika kushangilia ligi
zenu mbalimbali hivyo wanamichezo hamna budi kutu-azima mashabiki sauti
zenu katika kupinga ukatili na majanga mengine ya jamii,” alisema
Nyange.
Alifafanua kuwa kwa kuanzia wamechagua timu hizo tatu
ambapo baadaye tutatanua wigo kwa kushirikisha timu nyingine pale tu
watakapo kuwa tayari kujiunga nao.
Kwa mujibu wa Nyange, kampeni
hii itaanzia kwenye mikoa mine ambayo ni Mara, Mwanza,Dodoma na Dar es
Salaam. Alisema kuwa kampeni hiyo pia itatambulishwa rasmi mikao tofauti
kwa awamu. Alisema kuwa takwimu zinaonyesha kuwa mikoa hiyo ina vitendo
vingi viovu dhidi ya wanawake na watoto.
Aliongeza kusema kuwa
watatumia njia mbalimbali kufikisha ujembe huo ikiwa pamoja na mechi za
kirafiki, matukio ya jamii, na shughuli za elimu.
“Kampeni hii
inalenga kutoa maarifa kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na
watoto, na pia kuchochea mazungumzo kuhusu jinsi ya kuzuia na kukomesha
vitendo hivyo visivyo vya kibinadamu. Tunakaribisha kushiriki katika
kampeni hiyo muhimu, tunaamini kupitia umoja wetu, tunaweza kuleta
mabadiliko katika jamii yetu na kuwahakikishia wanawake na watoto ulinzi
wanayostahili,” alisema.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Naibu
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamis Mwinjuma ambaye alikuwa
mgeni tasmi, alivipongeza vilabu hivyo na kuoa rai kwa vilabu vingine
vya mpira wa miguu kuunga mkono kampeni hiyo.
Naibu Waziri
alisema kuwa mpira wa miguu ni mchezo namba moja nchini na una mashabiki
wengi na kama wachezaji na viongozi watashiriki katika kampeni za
kupinga ukatili kwa wanawake na watoto, jamii itabadilika na kuwa na
fikra chanya.
“Ni wakati wa kutumia nafasi zetu kuunga mkono
kampeni hizi ili jamii ibadilike, wachezaji na viongozi ni kioo cha
jamii na wote tukiungana, tutafikia malengo yetu,” alisema Mwinjuma.
Aliongeza
kwa kusema kuwa “Vita ya ukatili ni yetu sote, usalama na furaha ya
wanawake na watoto ndio chanzo cha maendeleo na amani ya sasa na kesho.
Nichukue nafasi hii kuviomba vilabu vingine vya mpira wa miguu kujiunga
na kampeni hii ya Piga Mpira Siyo Mwanamke. Tuunge mkono bidii za
serikali ya awamu ya sita na taasisi ya Thamani Women Tanzania kwa
mpango wake mahusisi wa kuondoa janga hili,”.
“Ni lazima vijana
wa kiume watambue ya kwamba katika janga hili wao ni suluhu na sio
tatizo tu kwa hivyo ni muhimu wajadili tatizo hili,” alisema.
Kwa
upande wake, Neema Tarimo ambaye ni Meneja Mradi wa Thamani Women
Tanzania alisema kuwa wamejipga vilivyo kufikisha ujumbe na kuhakikisha
kuwa kampeni hii inakamilika.
“Nachukua fursa hii kuwapongeza
viongozi wa timu hizi tatu na wadau kwa kutuunga mkono katika kampeni
hii muhimu kwa ustawi wa jamii, tunaamini tutafanikiwa,Tunakaribisha
kushiriki katika kampeni hiyo muhimu, tunaamini kupitia umoja wetu,
tunaweza kuleta mabadiliko katika jamii yetu na kuwahakikishia wanawake
na watoto ulinzi wanayostahili,” alisema Tarimo.
Tarimo
alifafanua kuwa kwa kwa njia ya mechi za kirafiki, matukio ya mbalimbali
ya kijamii, na shughuli za elimu, kampeni hii inalenga kutoa maarifa
kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, na pia kuchochea
mazungumzo kuhusu jinsi ya kuzuia na kukomesha vitendo hivyo visivyo vya
kibinadamu.
Wakati huo huo Mtendaji Mkuu wa Simba, Imani Kajula
alisema watatumia wachezaji wao na mitandao ya kijamii kupinga ukatili
wa wanawake na watoto kwa nguvu zote.
Kauli hiyo iliungwa mkono
na Ofisa Mtendaji Mkuu wa timu ya Azam FC, Abdulkarim Popat na wa
Singida Fountain Gates FC, Olebile Sikwane.
Naibu
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Khamis Mwinjuma “ Mwana FA) (wa
pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba
Imani Kajula (wa kwanza kulia),Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya
Thamani Women Tanzania Nafue Nyange (wa tatu kulia), Waziri Mkuu
Mstaafu John Malecela (wa tatu kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa klabu ya
Azam FC ,Abdulkarim Popat (wa pili kushoto) na Afisa Mtendaji Mkuu wa
klabu ya Singida Fountain Gate Olebile Sikwane wakati wa uzinduzi wa
kampeni maalum ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto
ijulikanayo kwa jina la Piga Mpira, Sio Mwanamke.
Naibu
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Khamis Mwinjuma “ Mwana FA
akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya kupinga ukatili
dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kwa jina la Piga Mpira, Sio
Mwanamke.
Mkurugenzi
mtedaji wa taasisi ya Thamani Women Tanzania Nafue Nyange akizungumza
wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya kupinga ukatili dhidi ya
wanawake na watoto ijulikanayo kwa jina la Piga Mpira, Sio Mwanamke.
Thursday, October 19, 2023

Home
HABARI
Thamani Women Tanzania, Simba SC, Azam FC na Singida FG kupinga ukatili dhidi ya wanawake, watoto
Thamani Women Tanzania, Simba SC, Azam FC na Singida FG kupinga ukatili dhidi ya wanawake, watoto
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment