HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 20, 2023

HESLB YATOA ORODHA YA WANAFUNZI KUNUFAIKA MKOPO WA ELIMU YA JUU AWAMU YA KWANZA 2023/2024

NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza awamu ya kwanza ya Wanafunzi 56,132 wa shahada ya kwanza waliopangiwa mikopo yenye thamani ya shilingi Bilioni 159.7 kwa mwaka wa Masomo 2023/2024.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Bw. Abdul-Razaq Badru amesema kuwa kati ya wanafunzi hao, wa kiume 32,264 sawa na asilimia 57% na wa kike ni 23,868 sawa na asilimia 43% na kuanzia leo wanaweza kuona taarifa za mikopo waliyopangiwa katika akaunti walizotumia kuomba mkopo.

Aidha Bw.Badru amesema kuwa maafisa wa HESLB watakuwa katika taasisi za elimu ya juu nchini kuanzia Jumatatu , Oktoba 23,2023 ili kuratibu usajili wa wanafunzi hao katika mfumo wa malipo.

"Kwa wanafunzi wapya, kama walivyoshauriwa wakati wa kuomba mkopo, wafike vyuoni wakiwa na namba za akaunti zao za benki, namba zao za simu zinazopatikana na watasajiliwa katika mfumo wetu wa malipo wa DiDiS baada ya kusajiliwa na Chuo'. Amesema Bw.Badru

Pamoja na hayo Bw.Badru amesema kuwa Serikali imetenga shilingi Bilioni 731 kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi 220,376, kati yao, wanafunzi 75,000 watakuwa ni wanufaika wa mwaka wa kwanza wa shahada ya kwanza na wanafunzi zaidi ya 145,376 ni wanaoendelea na masomo baada ya kufaulu mitihani yao ya mwaka.

Vilevile amewasihi waombaji wa mikopo wa shahada ya Kwanza, Stashahada na wanufaika wa 'Samia Scholrship' kwa mwaka 2023/2024 kuwa watulivu wakati taratibu za uchambuzi na upangaji wa mikipo na ufadhili kwa wanafunzi wenye sifa ukiendelea.

Kwa upande wake rais wa Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) Bi.Maria Thomas ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuongeza bajeti ya mikopo ambapo mwanzo ilikuwa Bilioni 654 hadi kufikia Bilioni 731.

Ameipongeza Bodi ya Mikopo kwa kuendelea kushirikiana nao katika kutatua changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanyiwa kazi.

Hata hivyo amewaomba wanaufaika wa mikopo watakapopata fedha zao, wazielekeze katika malengo mahususi katika kutimiza ndoto za elimu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) , Bw. Abdul-Razaq Badru (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) , Bw. Abdul-Razaq Badru (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) , Bw. Abdul-Razaq Badru akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) , Bw. Abdul-Razaq Badru akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) , Bw. Abdul-Razaq Badru akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) , Bw. Abdul-Razaq Badru (katikati) akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam.
rais wa Jumuiya ya Wanafunzi Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) Bi.Maria Thomas (wa kwanza kushoto) akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi wa upangaji na utoaji mikopo wa HESLB, Dkt. Peter Mmari akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam

Baadhi ya Watumishi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) wakifuatilia Mkutano wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) , Bw. Abdul-Razaq Badru na Waandishi wa habari leo Oktoba 20,2023 katika Ofisi za HESLB Jijini Dar es Salaam

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad