Baada ya kutembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa hospitali hiyo leo Jumamosi Oktoba 7, 2023, Komredi Chongolo ameahidi kwenda kuweka msukumo kwa serikali kuhakikisha wanapeleka haraka sh. bil. 5 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa mradi huo wa afya pamoja na kujenga jengo la kuhifadhia maiti hospitalini hapo.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Serafini Kisengi Patrice amesema kuwa kwa Mwaka wa Fedha 2023/24 Serikali imetenga jumla ya shilingi Bilioni 5,000,000,000 kwa ajili ya kuhakikisha ujenzi wa hospitali hiyo unakamilika kwa wakati ili wananchi wapate huduma zilizokusudiwa.
"Tunampongeza na Kumshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa hospitali hii,” amesema Dkt. Kisengi



.jpeg)



.
No comments:
Post a Comment