Benki
ya Standard Chartered kwa kushirikiana na SheFound wamewakutanisha
wanawake zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya
kujadili changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.
Wafanyabiashara
hao wanawake wamekutanishwa Novemba 23,2022 jijin Dar es es
salaam,ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered, Herman
Kasekende aliwakilishwa na Jerry Agyeman-Boateng.
Akitoa
maoni yake kwa niaba ya Benki, Jerry Agyeman-Boateng ambaye ni Mkuu wa
Biashara Wateja Wakubwa, wa Kati na Taasisi za Fedha amesema lengo lao
ni kuendesha biashara na ustawi kupitia utofauti wao wa kipekee.
Aidha
amesema katika enzi ya kisasa ya kidijitali, wahalifu wa mtandao
wanazidi kulenga mashirika mengi. Shirika lolote linaweza kulengwa na
wahalifu wa mtandao iwapo hawatadhibitiwa ipasavyo .Tuna jukumu la
kutekeleza ili kuhakikisha tunafahamishwa vyema kuhusu mashambulizi ya
mtandaoni yanayoweza kutokea ili tunapofanya biashara tuwe salama."
Hivyo
amesema benki hiyo inaishukuru SheFound kwa kushirikiana nayo kwenye
kuwajengea uelewa wanawake kuhusu masuala ya usalama kwenye mitandao.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa SheFound Vannesa Kisowile pamoja na
mambo mengine ameeleza kwamba zaidi ya asilimia 60 ya mandhari ya MSME
barani Afrika yanaundwa na wanawake wajasiriamali kwa kutumia
teknolojia.
Amesema
ni muhimu kuongeza ufahamu kuhusu mambo ya usalama wa mtandao ili
kupunguza matukio ya wizi yanayofanyika mtandaoni."Hii itasababisha
ukuaji na uendelevu wa biasharapamoja na maendeleo ya jumla ya kijamii
na kiuchumi."
Pia
kulikuwa na mjadala ulihusisha wadau wengine wakiwemo wabobezi kwenye
mambo ya biashara na tehama ambao walishiriki kutoa elimu na
kubadilishana ujuzi na maarifa na wafanyabiashara hao.
Akizungumzia
dhamira ya Benki ya kusaidia wanaoanza biashara, Busara Raymond ambaye
ni Meneja wa Bidhaa za Fedha katika Benki ya Standard Chartered amesema
Benki imewezesha kusaidia uanzishaji wa biashara kupitia SC Ventures
ambacho ni kitengo cha biashara kinachohusika kuchochea na kukuza
uvumbuzi. Pia kuwekeza kwenye teknolojia ya kifedha na kuchunguza mifumo
mbadala ya biashara. SC Ventures iko wazi kwa biashara zote
zinazoanzishwa ambazo zina maoni ya kibiashara yanayofaa.
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Tehama Tanzania, Dkt Nkundwe Mwasaga akizungumza kwenye
moja ya kongamano lililoandaliwa na Benki ya Standard Chartered kwa
kushirikiana na taasisi ya SheFound ambapo liliwakutanisha wanawake
zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kujadili
changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Tehama Tanzania, Dkt Nkundwe Mwasaga (wa tatu kulia)
akizungumza kwenye moja ya kongamano lililoandaliwa na Benki ya Standard
Chartered kwa kushirikiana na SheFound ambapo liliwakutanisha wanawake
zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kujadili
changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.Mtaalamu
wa masuala ya 'IT' na Mhamasishaji wa Jamii kuhusu masuala ya Kifedha
kutoka Benki ya Standard Chartered Bupe Mwakabaga akieleza jambo kwenye
kongamano hilo lililoandaliwa na Benki ya Standard Chartered kwa
kushirikiana na taasisi ya SheFound ambapo liliwakutanisha wanawake
zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kujadili
changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.Pichani
kushoto ni MKurugenzi wa Kampuni ya ya Meriitech Esther Mwasaga
Baadhi ya washiriki wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye kongamano hilo
No comments:
Post a Comment