Ikiwa ni
mwendelezo wa kuadhimisha mwezi wa huduma kwa wateja, wafanyakazi 6 wa
Benki ya NMB jana wameanza safari ya siku 7 ya kupanda Mlima Kilimanjaro
kupitia geti la Machame ambapo wataipeperusha bendera ya benki hiyo
katika kilele cha mlima huo.
Akizungumza katika hafla ya kuwaaga
na kuwakabidhi rasmi bendera wafanyakazi hao, Ofisa Mkuu wa Hifadhi ya
Taifa ya Mlima Kilimanjaro(KINAPA), Charles Ng'endo alisema kama Hifadhi
ya KINAPA wamefarijika sana na utaratibu iliofanywa na NMB katika
kuadhimisha mwezi huu muhimu wa huduma kwa wateja kwa kupanda Mlima
Kilimanjaro, aidha wao kama hifadhi watahakikishia kuwa wamewawekea
mazingira mazuri na utaratibu mzuri wa kuwahudumia mpaka wanafika
kileleni.
Aliongeza kuwa “kufanya hivi kunatusaidia kutangaza
utalii wa ndani na tunafahamu hifadhi ya Taifa TANAPA na NMB tumekuwa na
mahusiano ya karibu ya kibiashara na kiutoaji wa huduma kwa wananchi.
Hivyo, kupanda Mlima Kilimanjaro na kufika kileleni kutaimarisha
mahusiano kati yetu sote na kupeleka ujumbe kwa wateja wetu kuweza
kutangaza utalii wa ndani,"
Nae Meneja wa benki hiyo Kanda ya
Kaskazini-Dismas Prosper alisema kuwa, NMB kwa kutambua umuhimu wa sekta
ya Utalii hapa nchini, waliona ni jambo la kifahari kusherekea mwezi wa
huduma kwa wateja pamoja na wateja wao ambao wapo katika hii kwa
kupandamlima Kilimanjaro ili kuutangaza mlima huo. Timu hiyo
imepandishwa Mlima na kampuni ya Zara tours yenye uzoefu wa miaka mingi.
Akimalizia kuzungumza, kiongozi wa msafara huo wa wafanyakazi
wa NMB ambaye pia ni Afisa Mkuu wa Wateja Wakubwa wa NMB – Alfred Shao
alisema kuwa, NMB imefanya mambo mengi makubwa hapa nchini ikiwamo kuwa
Benki bora na yenye masuluhisho mengi ya kifedha kwa wateja wao na
kwamba wanataka kuwadhihirishia umma na wateja wao kuwa wanao uwezo wa
kuwahudumia mpaka kilele cha Mlima Kilimanjaro na wajue wanamaanisha
wanaposema ‘NMB Karibu Yako’.
Wengine waliopanda Mlima ni Nishad Jinah, Stella Motto, Reginald Baynit, Agnes Mlolele na Christopher Mwalugenge
Msafara wa wafanyakazi wa NMB wanaopanda Mlima Kilimanjaro wakiwa katika picha ya pamoja na wenzao wa Matawi ya Moshi, waliofika kuwatakia kila la kheri kabla ya safari yao ya siku 7.
No comments:
Post a Comment