HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 22, 2022

WAZIRI SIMBACHAWENE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI TENDAJI MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. George Simbachawene akiongoza kikao cha Pili cha Kamati Tendaji Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa, kikao kilifanyika Julai 22, 2022 katika Ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dodoma.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio (katikati), Naibu Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Ramadhani Kailima (wa kwanza kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Stella Joseph wakifuatilia kikao hicho.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Kaspar Mmuya akizungumza jambo wakati wa kikao cha Pili cha Kamati Tendaji Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho wakikagua ratiba ya maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa wakati wa kikao cha maandalizi.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Maadhimisho na Sherehe za Kitaifa Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Batholomeo Jungu akifafanua jambo wakati wa kikao hicho

Baadhi ya wajumbe wa kikao cha Kamati Tendaji ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa wakifuatilia kikao hicho.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad