HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 10, 2022

MASALA PRINCESS WAANZA KWA KISHINDO LIGI YA WANAWAKE MKOA WA DAR ES SALAAM, YASHINDA 14-1

 

Na Said Mwishehe, Michuzi TV

KUMENOGA! Hivyo ndivyo unavyoweza kuelezea baada ya timu ya Masala Princess Girls kuibuka na ushindi wa mabao 14-1 dhidi ya timu ya Ukonga katika Ligi ya wanawake ya Mkoa wa Dar es Salaam inayoratibiwa na Shirikisho la mpira Tanzania (TFF)

Ligi hiyo imeanza rasmi leo Juni 9,2022 katika Viwanja vya Karume jijini Dar es Salaam ambapo timu 10 zinashiriki ligi hiyo.

Katika mchezo wa leo kwenye ligi hiyo timu ya Masala Princes Girls imeibuka na ushindi huo mnono baada ya kuifunga timu ya Ukonga katika Ligi ya wanawake ya Mkoa wa Dar es Salaam na mchezo ulikuwa wa kuvutia sana kutokana na uwezo waliokuwa wakionesha wachezaji wa timu zote mbili.
 

Hata hivyo umahiri wa wachezaji wa Masala Princes Girls uliifanya timu hiyo kuonekana moto wa kuotea mbali wakati wote wa mchezo huku wapinzani wao wakionekana kuzidiwa licha ya kufanya tihada za kutaka kupata matokeo mazuri.

Awali kabla ya kuanza kwa mchezo huo wa ufunguzi wa ligi hiyo inayokwenda sambamba na utoaji wa elimu kwa mtoto wa kike kuhusu masuala mbalimbali Meneja Programu za Vijana CIS Ester Mpanda amesema kwenye shirika lao kuna program ya vijana wa kike inayoitwa

Girls Talk, Girls Power.
“Mwaka huu tuko kwenye Program ya afya na michezo na kupitia program hiyo tumeanzisha timu ya michezo ya Watoto wa Kike inayoitwa Maisala Princes ambayo leo imefanikiwa kucheza ligi ya wanawake ya Mkoa wa Dar es Salaam.

“Kwa kweli kama CSI CSI mashindano haya ni kitu kikubwa kwetu kwasababu watoto wa kike wanafanya vizuri sana na katika mashindano haya ni mashindano makubwa, tunazo timu 10 zinazoshiriki na zimekuwa zikifanya vizuri sana katika Mkoa wa Dar es Salaam.

“Mshindi wa mashindano haya atakwenda kuuwakilisha mkoa wa Dar es Salaam katika mashindano yatakayoshirikisha mikoa yote ya Tanzania yatakayofanyika Dodoma,”amesema Mpanda huku akifafanua atakayeibuka mshindi katika mashindano ya mikoa yote atakuwa amefuzu ligi daraja la kwanza.

“Niwashukuru wadau wa mpira wa kike, niwashukuru watu wanaotusaidia Abec Company, tunatoa shukrani kwa CSI ambao wamekuwa na programu mbalimbali ambazo zimejikita kutoa elimu kwa mtoto wa kike,”amesema.

Amefafanua CSI wamekuwa na program nyingi lakini program ya Girls Talk ,Girsl Power inaonesha kupokelewa vema na Watanzania, hivyo wataendelea kusimamia vema mashindano hayo huku akitoa shukrani kwa Mkuregenzi Mkazi wa CSI Stella Mpanda pamoja na Mkurugenzi na Mwakilishi wa CSI Tausi Kagasheki anayeishi nchini Marekani.

“Tumekuwa tukifanya kazi kama timu na kila kitu naamini kabisa ni mipango ya Mungu, tumeanza na programu nyingi lakini hii tunaamini inakwenda kufanya vitu vikubwa na mabadiliko makubwa hasa kwa mtoto wa kike , nishukuru sana Tanzania, niishukuru TFF tu natamani kuona hawa watoto wanacheza mpaka nje ya nchi,”amesema Mpanda.












































No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad