WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa jana Mei 25, 2022 amepokea mapendekezo kutoka kwa
wananchi wa Tarafa za Loliondo, Ngorongoro na Sale kuhusu namna bora ya
kulinda uhifadhi wa maeneo hayo.
Maoni
hayo yaliwasilishwa kwa Waziri Mkuu na wawakilishi wa wakazi wa wilaya
hiyo wakiwemo Mbunge wa Ngorongoro Mhe. Emmanuel Shangai, Malaigwanani,
Madiwani, wenyeviti wa vijiji, wawakilishi wa wanawake na vijana,
ofisini kwake Mlimwa, Dodoma.
Baada
ya kupokea mapendezo hayo, Waziri Mkuu aliwasisitiza wananchi hao
waendelee kuiamini Serikali yao kwani haiwezi kuwa na mipango mibovu kwa
wananchi wake. “Msisikilize maneno maneno ya watu wa pembeni.”
Akizungumzia
kuhusu eneo la Msomera lililoko wilayani Handeni, Tanga ambako
yanaandaliwa makazi kwa ajili ya kuwahamishia wakazi wa Ngorongoro
waliokubali kuhama kwa hiari alisema ujenzi unandelea vizuri.
Waziri
Mkuu alisema ujenzi wa nyumba za makazi 103 upo mbioni kukamilika na
pia, Serikali imepanga kuongeza nyumba nyingine lengo likiwa ni kufikia
nyumba 500 kwa ajili ya wakazi hao.
Kadhalika,
Mheshimiwa Majaliwa alisema Serikali inaendelea kuimarisha sekta ya
mifugo ili kuhakikisha wafugaji wote nchini wanapata tija kupitia
shughuli hiyo.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Laigwnani Metui Ole Shaudo
mapendekezo ya Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro kuhusu namna bora ya
kudumisha Hifadhi ya Ngorongoro wakati alipokutana na Mbunge wa
Ngorongoro Emmanuel Shangay Malaigwani, Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji
pamoja na wawakilishi wa wanawake na Vijana kutoka wilaya ya Ngorongoro,
ofisini kwa Waziri Mkuu,Mlimwa jijini Dodoma,
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Laigwnani Lawrance Ngorisa
mapendekezo ya Wananchi wa Tarafa za Loliondo na Sale wilayani
Ngorongoro kuhusu namna bora ya uhifadhi wakati alipokutana na Mbunge wa
Ngorongoro Emmanuel Shangay, Malaigwani, Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji
pamoja na wawakilishi wa wanawake na vijana wa tarafa za wilaya hiyo,
ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma,
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Madiwani, wenyeviti wa Vijiji,
Mbunge wa Ngorongoro Emmanuel Shangay pamoja na wawakilishi wa vijana na
wanawake wakati alipopokea mapendekezo ya wananchi wa Tarafa za
Ngorongoro, Loliondo na Sale wilayani Ngorongoro kuhusu namna bora ya
uhifadhi kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma.
Baadhi
ya Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji na wawakiizshi wa wanawake na vijana
wa Tarafa za Ngorongoro, Loliondo na Sare wilayani Ngorongoro
wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipozungumza nao baada ya
kupokea mapendekezo ya Wananchi wa Tarafa hizo kuhusu namna bora ya
uhifadhi kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Malaigwanani
kutoka Tarafa za Ngorongoro, Loliondo na Sale wilayani Ngorongoro baada
ya kupokea mapendekezo ya mwananchi kuhusu namna bora ya uhifadhi katika
tarafa hizo, ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Mei 25,
2022. Kulia wake ni Mbunge wa Ngorongoro, Emmanuel Sangay na kushoto
wake ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Ngorongoro, Ndirango Ole Senge.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa
wanawake kutoka Tarafa za Ngorongoro, Loliondo na Sale wilayani
Ngorongoro baada ya kupokea mapendekezo ya mwananchi wa Tarafa hizo
kuhusu namna bora ya uhifadhi katika tarafa hizo, ofisini kwa Waziri
Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Mei 25, 2022. Kulia wake ni Mbunge wa
Ngorongoro, Emmanuel Sangay na kushoto wake ni Mwenyekiti wa CCM wa
wilaya ya Ngorongoro, Ndirango Ole Senge. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
No comments:
Post a Comment