Benki ya NMB imetenga Sh.
bilioni moja kwaajili ya kuwasaidia wabunifu wachanga waweze kuimarika
na kuzifanya bunifu zao kuwa bora na zenye manufaa kwa uchumi wa Taifa
kwa ujumla.
Hayo yameelezwa na Meneja Idara ya Utafiti wa Benki
ya NMB, Prochest Kachenje alipokuwa anamuelezea Naibu Waziri wa Elimu,
Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Juma Kipanga alipotembelea banda la
NMB wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Tafiti na Ubunifu ya chuo kikuu cha
Dar es Salaam.
“NMB imetenga shilingi bilioni moja kwaajili ya
kuwasaidia wabunifu wanaochipukia kuweza kuziweka bunifu zao katika
utekelezaji ili waweze kunufaika”
“Mwaka jana tulizindua mfumo
maalumu wa NMB Sandbox Environment ambapo wabunifu wa suluhishi
mbalimbali za kifedha wanaweza kufanya majaribio ya bunifu zao na kwa
zitakazo fuzu, tutashirikiana nao,” aliongezea Prochest.
Lakini
pia, Prochest alisema kuwa kiasi hiki cha fedha sio mkopo bali ni fedha
iliyotengwa kwa dhumuni ya kusaidia wabunifu hawa na hawatawajibika
kuirejesha.
Alitumia pia fursa hiyo kuwakaribisha wanachuo na
Vijana wabunifu kuishirikisha Benki ya NMB juu ya bunifu zao ili
kuwasaidia kupata fedha za kuboresha zaidi.
Meneja
wa utafiti wa Benki ya NMB, Prochest Kachenje akizungumza na Naibu
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Juma Kipanga
alipotembelea banda la NMB wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Tafiti na
Ubunifu – Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Maafisa wa benki ya NMB kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Tafiti na Ubunifu – Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment