Mwenyekiti
wa Bodi ya NMB Foundation, Ruth Zaipuna (wa pili kushoto), akizindua
rasmi dirisha la kupokea maombi ya ufadhili wa wanafunzi wanaotegemea
kuingia kidato cha tano mwaka huu na wale wanaotarajia kuingia vyuo
vikuu kwa ajili ya shahada ya kwanza ya masomo. Kushoto ni mjumbe wa
Bodi, Juma Kimori na kulia ni Katibu wa NMB Foundation, Consolata Mosha
na mjumbe wa Bodi, Filbert Mponzi.
Taasisi
ya NMB Foundation imetangaza kuanza rasmi utaratibu wa kutoa ufadhili
wa masomo kwa wanafunzi wa kidato cha tano, sita na elimu ya juu baada
ya programu hiyo kuzinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mwishoni mwa
mwaka jana
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es
Salaam leo, Mwenyekiti wa Bodi ya NMB Foundation, Ruth Zaipuna amesema
wameanza kupokea maombi kupitia matawi yote ya benki hiyo yaliyopo nchi
nzima na tovuti ya NMB Foundation.
“Kwa kuanzia tutatoa ufadhili
kwa wanafunzi 200, ambapo 150 watakuwa wa kidato cha tano na sita,
wanafunzi 50 watakuwa wa elimu ya juu. Fadhili utalipia gharama zote za
masomo ikiwemo ada, fedha za kujikimu, vifaa na mahitaji mengine
yatakayotajwa kweye fomu ya kujiunga na shule au chuo,” amesema Ruth.
Alifafanua
kuwa kwa wanfunza wa sekondari watakaopata ufadhili watalipiwa ada,
nauli, vifaa vya kujifunzia, fedha za kujikimu, bima ya afya na mahitaji
mengie watakayotakiwa kutoka shule. Kwa upande wa elimu ya juu,
wanafunzi watalipwa ada, fedha za kujikimu, fedha za mafunzo kwavitedo,
Laptop na gharama nyingine watakazotakiwa kwenye fomu ya kujiunga na
chuo.
Aidha, Zaipuna alisema wamejipanga kuweka masomo ya
vipaumbele kwa wanafunzi watakaopata fursa ya udhamini. Lengo ni
kuhakikisha wanashiriki mabadiliko ya kijamii na kiuchumi kupitia malezi
na mafunzo watakayopata wanafunzi hao.“
Tutaangalia kwa kina
masomo ya takwimu na mahesabu, biashara na uchumi, Teknolojia ya
Mawasiliano ya Umma, uhandisi, mafuta na gesi pamoja na sayansi na
teknolojia,” alibainisha Zaipuna na kuongeza:
“Nina imani kupitia
programu hii tutaibua vipajij na tutatimiza ndoto za vijana. Kadiri
tutakavyoendelea idadi ya wanafunzi watakaonufaika itaongezeka kulingana
na mahitaji ambapo tutapanua wigo wa wadau wengine watakaotaka
kushirikiana nasi kwenye jambo hili muhimu kwa maendeleo ya nchi.”
Katika
hatua nyingine, Ruth alisema NMB Foundation itahakikisha watu
watakaohusika kukusanya na kupitisha wanafunzi wanaofaa kwa kupewa
ufadhili watakuwa makini kutimiza vigezo, ambapo kwa wale watakaokwenda
kinyume na utaratibu watachukuliwa hatua za kinidhamu.
“Tunataka
kulifanya zoezi hili liwe na uwazi na ukweli, ndio maana tumesema
tutawashirikisha hata viongozi wa serikali za mitaa kuanzia kata hadi
mitaa, lengo ni kuhakikisha wanufaika watakaopatikana ni kweli wana
vigezo vinavyohitajka,” alisisitiza Zaipuna.
No comments:
Post a Comment