HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 20, 2022

ENGENI MAZINGIRA RAFIKI YATAKAYOMUWEZESHA MWANAFUNZI KUSOMA

 




Na Janeth Raphael - Dodoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ameigiza Wizara ya Elimu kuhakikisha inaendelea kujenga mazingira rafiki yatakayowezesha wanafunzi kupenda zaidi kusoma masomo ya sayansi na teknolojia pamoja na kuendelea kufanya mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 na kubadilisha mitaala ili kuongeza ubora wa elimu na mafunzo.

Dkt Mpango ametoa agizo hilo leo Mei 19,2022 wakati akifunga maonesho ya wiki ya ubunifu yanayokwenda sambamba na Mashindano ya Ubunifu wa Sayansi na Teknolojia(MAKISATU) kwa mwaka 2022 ambayo yameandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo(UNDP) kupitia mradi wake wa FUNGUO yaliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.


Makamu wa Rais ameitaka Wizara ya Elimu kuendelea kutafuta fursa za masomo kwa kwa watanzania katika vyuo bora duniani katika nyanja za sayansi, teknolojia na tiba kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020.

'Wizara inapaswa kuwafuatilia kwa karibu wanafunzi wabunifu na kuhakikisha wanaendelezwa ili waweze kuwa msaada katika utatuzi wa changamoto mbalimbali kwa kutumia teknolojia. 'amesema Dkt Mpango

Hata hivyo amesema kuwa familia zina wajibu wa kuwahamasisha na kuwatia moyo watoto wanapokuwa na mawazo ya kibunifu pamoja na kuwaunga mkono katika kupenda elimu ya sayansi.

Dkt Mpango amesema mashindano ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu yanapaswa kufanyika katika mikoa yote.

Aidha ameiagiza Wizara ya Elimu kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuhakikisha Halmashauri zinatenga maeneo maalum ya kuanzisha vituo vya ubunifu na atamizi za kisekta kulingana na shughuli za kiuchumi katika maeneo husika kwa ajili ya kulea vijana wenye ubunifu, ugunduzi na maarifa asilia.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais ameitaka taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kuhamisha maarifa ya tafiti katika vitendo. Amewataka kuendelea kutambua mazao yanayoweza kuwasaidia wakulima hasa wale wa chini kwa urahisi zaidi kulingana na mvua zinazopatikana katika mkoa husika.

Kwa Upande wake Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa amesema serikali ya awamu ya sita imedhamiria kwa dhati kuwahudumia wabunifu ili mawazo na ubunifu uweze kutumika na jamii ya watanzania. Aidha amezita taasisi zinazohudumia wabunifu kujipanga vizuri pamoja na kutoa elimu kwao ikiwemo kuwasaidia kulinda hati miliki zao.

Awali Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda amesema serikali kupitia Buni Hub na DTBI imewezesha kuanzishwa kwa makampuni zaidi ya 94 yaliotokana na ubunifu na kutoa ajira kwa vijana zaidi ya 30000.

Aidha Prof Mkenda amesema mchango wa kampuni hizo katika pato la taifa umeanza kuonekana kutoka na baadhi ya kampuni hizo kuchangia zaidi milioni 500 kwa mwaka kila mmoja.


 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad