Makamu wa Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango leo tarehe
25 Mei 2022 ameshiriki katika majadiliano maalum ya viongozi wakuu wa
nchi za Afrika katika ajenda iliohusu namna Bara la Afrika linavyoweza
kubadili utaratibu wa kimataifa katika kukabiliana na masuala mbalimbali
,majadiliano yaliofanyika katika mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani
unaoendelea Davos nchini Uswisi.
Akizungumza katika majadiliano
hayo, Makamu wa Rais amesema ni muhimu nchi za Afrika kushirikiana
katika kuwezesha tafiti za ndani ya nchi ili kukabiliana na majanga
mbalimbali yanapojitokeza pasipo utegemezi. Makamu wa Rais ameitaja
taasisi ya Taifa ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR) iliopo nchini Tanzania
pamoja na taasisi zingine za ndani ya nchi zilitoa msaada mkubwa wakati
wakati wa kukabiliana na Uviko 19. Amesema ni muhimu kushirikiana na
sekta binafsi zilizopo ndani ya nchi kwani zimekua zikitoa mchango
mkubwa hasa wakati wa kukabiliana na majanga mbalimbali.
Aidha
Makamu wa Rais amesema kwa kutumia rasilimali zilizopo, mataifa ya
Afrika yanaweza kukabiliana na changamoto zinazojitokeza na kuongeza
kwamba kwa sasa Tanzania inazalisha chanjo ya mifugo hivyo hakuna budi
mataifa ya Afrika kuungana katika uzalishaji huo utakaosaidia mahitaji
ya baadae.
Mkutano huo umeshirikisha viongozi wakuu wa Nchi na Serikali za Afrika pamoja na wawakilishi kutoka mataifa hayo.
Makamu
wa Rais Dkt. Philip Mpango anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa Jukwaa la
Uchumi Duniani unaofanyikia Davos nchini Uswisi unaoshirikisha wakuu wa
nchi, wakuu wa taasisi na mashirika ya kimataifa pamoja na
wafanyabiashara.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango
akizungumza wakati wa majadiliano maalum ya Viongozi Wakuu wa Nchi za
Afrika katika Ajenda ya namna Bara la Afrika linavyoweza kubadili
utaratibu wa kimataifa katika kukabiliana na masuala mbalimbali,
majadiliano yaliofanyika katika mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani
unaoendelea Davos nchini Uswisi. Mei 25,2022
Wednesday, May 25, 2022

Home
HABARI
MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI MAJADILIANO MAALUM YA VIONGOZI WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA DAVOS NCHINI USWIZI
MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI MAJADILIANO MAALUM YA VIONGOZI WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA DAVOS NCHINI USWIZI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment