HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, May 15, 2022

MAELEKEZO YA SHAKA KWA WANAOTEKELEZA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA, ATAKA MAZINGIRA RAFIKI KWA WAMACHINGA...MGAMBO WAONYWA

 


Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Manyara

CHAMA Cha Mapinduzi( CCM) kimewaelekeza watendaji wenye dhamana wa serikali kushuka ngazi za chini na kuzisikiliza changamoto na kero zinazowakabili wananchi na kuzipatia utatuzi huku akikitoa rai kwa viongozi kutekeleza maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan bila kuathiri shughuli zinazofanywa na wananchi katika kujitafutia kipato.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa Chama hicho Shaka Hamdu Shaka ameleeza hayo wakati akizungumza na wajasiriamali wadogo na wakati wakiwemo Machinga, Mama Lishe na waendesha bodaboda eneo la Stendi ndogo ya Mabasi Babati Mjini.

Shaka baada ya kufika kwenye stendi hiyo alipata nafasi ya kusikiliza wananchi akiwa kwenye kijiwe cha kuuza Kahawa ambapo miongoni mwa malalamiko aliyopewa ni uwepo wa manyanyaso yanayofanywa na baadhi ya mgambo kwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga.

“Si vema kwa watendaji wenye dhamana wa serikali kuu na serikali za mitaa kujiweka mbali bila kufuatilia matatizo yanayowakera wananchi kwa kupata bughudha mbalimbali ikiwemo mgambo wa halmashauri za wilaya, manispaa na miji midogo na majiji wanaowanyanyasa wajasirimali wajapokuwa katika shughuli zao za uzalishaji mali.

“ Lengo la Rais Samia Suluhu Hassan kuagiza wafanyabiashara ndogo ndogo wapangwe Chama Cha Mapinduzi tunaliunga mkono kwa asilimia 100, tunataka kuona wafanyabiashara wanakaa katika maeneo salama na kufanya biashara zao bila kusumbuliwa.

“Tunashauri wenzetu wa Serikali kutekeleza maelekezo ya Rais kwa kuhakikisha maeneo ya kufanya biashara yanakuwa rafiki , tunataka kuona wafanyabishara wanaongezeka mitaji yao , hatutaki kuona wafanyabiashara wanafilisika kibiashara, tunataka wakuze biashara zao kwa kuhakikisha wanawekewa mazingira rafiki,” amesema Shaka.
kila siku,” amesema Shaka.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi Taifa akiwa kwenye kijiwe hicho cha kahawa amepata nafasi ya kusikiliza kero za wananchi na kupitia hekima,busara alizonazo ametoa utatuzi wa changamoto hizo hali iliyofanya kuibua shangwe kwa wananchi wanyonge hasa wanaojihusisha na biashara ndogondogo.

Shaka amesema kuwa kazi ya CCM ni kuisikiliza wananchi na wakishasikiliza wanatafuta ufumbuzi kwa kuishauri Serikali namna nzuri ya kushughulikia matatizo ya wananchi, huku akieleza pamoja na uwepo wa sheria na taratibu bado kuna kila sababu ya viongozi kutumia sahihi kutafuta suluhu bila kuharibu shughuli za watu.

Awali mmoja ya wajasiriamali mdogo anayejihusisha na uuzaji wa matunda na mbogamba akizungumza kwa niaba ya wajasiriamali wengine wadogo hasa wanawake kueleza kwamba katika zoezi la kupanga wamachinga katika maeneo ya Babati yamewaweka katika mazingira magumu kibiashara, hivyo wanaomba waruhusiwe kufanya biashara nyakati za usiku.

Amesema kuwa walikopelekwa sio mazingira rafiki kwa kufanyabiashara kwani ni eneo ambalo wamewekwa pamoja na wafanyabishara ambao ni wakulima wanaokuja kuuza mazao, hivyo wao kushindwa kuuza ukizingatia wengi wao wamekopa na wanaendesha maisha yao kwa kutumia biashara hizo ambazo nyingi ni za kuuoza haraka iwapo watashindwa kuuza kwa wakati.

Aidha wafanyabiashara wengine kwenye stendi hiyo ya zamani wametoa ombi kwa Shaka kuwaombea kwa viongozi wa Serikali kama itawezekana daladala zirudishwe eneo hilo kwani biashara zao zimekuwa ngumu kidogo huku wakizungumzia umuhimu wa kuboreshwa eneo hilo.







No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad