Kamishna
Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee akiendesha
trekta na akikagua trekta jipya aina ya John Deer HP 110. CGP Mzee
amewapongeza Viongozi wa Mkoa wa Katavi na Gereza KalilanKulukulu kwa
kununua trekta hilo lililogharimu Tshs 110 milioni.
Moja
ya nyumba za makazi ya askari Gereza la Kilimo Mollo, Rukwa ambayo
imejengwa kwa njia ya kujitolea. Aidha, Kamishna Jenerali wa Magereza,
Meja Jenerali Suleiman Mzee Mzee ameagiza uongozi wa Gereza hilo
kuanzisha Kilimo cha umwagiliaji.
Muonekano
wa nyumba za Maafisa na askari Gereza Kalilankulukulu mkoani Katavi
zikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi. CGP Mzee amepongeza ujenzi wa
nyumba hizo ambazo ni zaidi ya kumi kwa njia ya kujitegemea.
Kamishna
Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee akikagua matofali ya
"interlocking blocks" yanayotumika katika ujenzi wa nyumba za askari
Gereza Kalilankulukulu.
Kamishna
Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee akizindua jengo la
Ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoani Katavi leo Mei 15, 2022. Jengo hilo
limejengwa kwa njia ya kujitegemea.
Muonekano wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoani Katavi baada ya kuzinduliwa na CGP - Suleiman Mzee.
Maafisa
na askari wa Gereza Kalilankulukulu wakionesha shughuli mbalimbali
zinazofanyika katika Gereza hilo mara baada ya Mkuu wa Jeshi la
Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee kuwasili katika Gereza hilo kwa
ziara ya kikazi leo Mei 15, 2022.
Kamishna
Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee(katikati) akiwa
katika picha ya pamoja na maofisa na askari wa Gereza Songwe
alipotembelea Gereza hilo. Picha zote na Jeshi la Magereza.
No comments:
Post a Comment