Mkuu
wa Kitengo cha wateja binafsi wa Benki ta CRDB, Stephen Adili (wa tatu
kulia) akimkabidhi Kamishna wa Utawala na Fedha Jeshi la Zimamoti,
Mbaraka Semwanza (wa tatu kushoto), sehemu ya vifaa vya Studio na
Tehama, vitakavyotumiwa na Jeshi la Zimamoto kutoa taarifa mbalimbali
kwa Umma, katika hafla fupi ya makabidhiano hayo iliyofanyika kwenye
Ofisi za Jeshi hilo, Ilala jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka
kulia ni Meneja Mwanadamizi wa Huduma Mbadala Benki ya CRDB, Mangire
Kibanda, Meneja Mwandamizi wa Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Farida
Hamza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Zimamoto, Puyo
Nzalayamisi pamoja na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Ilala,
Mrakibu Elisa Mugisha.
Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi wa Benki ta CRDB, Stephen Adili (wa
tatu kulia) akimkabidhi Kamishna wa Utawala na Fedha Jeshi la Zimamoti,
Mbaraka Semwanza (wa tatu kushoto), sehemu ya vifaa vya Studio na
Tehama, vitakavyotumiwa na Jeshi la Zimamoto kutoa taarifa mbalimbali
kwa Umma, katika hafla fupi ya makabidhiano hayo iliyofanyika kwenye
Ofisi za Jeshi hiyo, Ilala jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka
kulia ni Meneja Mwanadamizi wa Huduma Mbadala Benki ya CRDB, Mangire
Kibanda, Meneja Mwandamizi wa Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Farida
Hamza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Zimamoto, Puyo
Nzalayamisi pamoja na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Ilala,
Mrakibu Elisa Mugisha.
Kamishna
wa Utawala na Fedha Jeshi la Zimamoti,
Mbaraka Semwanza akijaribu moja ya vifaa hivyo vilivyotolewa na Benki ya
CRDB, vitakavyotumiwa na Jeshi la Zimamoto kutoa taarifa mbalimbali
na elimu kwa umma juu ya majanga ya moto. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha
wateja binafsi wa Benki ta CRDB, Stephen Adili.
Mkuu
wa Kitengo cha wateja binafsi wa Benki ta CRDB, Stephen Adili
akizungumza na waandishi wa habari katika hafla fupi ya makabidhiano ya
vifaa vya Studio na
Tehama, vitakavyotumiwa na Jeshi la Zimamoto kutoa taarifa mbalimbali
na elimu kwa umma juu ya majanga ya moto, iliyofanyika kwenye
Ofisi za Jeshi hiyo, Ilala jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni
Kamishna wa Utawala na Fedha Jeshi la Zimamoti,
Mbaraka Semwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Zimamoto,
Puyo
Nzalayamisi pamoja na Meneja Mwandamizi wa Wateja Binafsi Benki ya CRDB,
Farida
Hamza.
Kamishna wa Utawala na Fedha Jeshi la Zimamoti,
Mbaraka Semwanza akizungumza wakati akitoa shukrani wa Benki ya CRDB, baada ya kupokea vifaa vya Studio na
Tehama, vitakavyotumiwa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoa taarifa mbalimbali
na elimu kwa umma juu ya majanga ya moto, katika hafla iliyofanyika kwenye
Ofisi za Jeshi hiyo, Ilala jijini Dar es salaam.
Benki
ya CRDB imetoa msaada wa vifaa vya Studio na Tehama kwa Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji, ikiwa ni kuliongezea nguvu Jeshi hilo katika utoaji wa taarifa mbalimbali
na elimu kwa umma juu ya majanga ya moto nchini, katika hafla iliyofanyika kwenye Ofisi za Jeshi hiyo, Ilala jijini Dar es salaam.
Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya CRDB, Stephen Adili,
alisema wamemeamua kulisaidia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili
kurahisisha mawasiliano na kuwawezesha wananchi kufikiwa na taarifa
zinazohusu maswala mbalimbali ya Zimamoto na Uokoaji popote na
wanapokuwa na wakati wowote.
Vifaa
hivyo vilivyotolewa ni pamoja na Kompyuta mbili aina ya iMac na Mac
book Pro, Televisheni Hisense 55", Vifaa vya Studio pamoja na kamera
aina Canon Mark IV 5D, vyote vikiwa ni vifaa vya kisasa kabisa ili
kuendana na hali ya sasa katika teknolojia.
Akipokea Msaada huo, Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi hilo, Mbaraka Semwanza alisema msaada huo utakuwa chachu kwa wanahabari wa Jeshi kuhakikisha Elimu ya Kinga na Tahadhari inaufikia Umma kwa kiwango kikubwa tofauti na hapo awali.
Kamishna
Semwanza kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
ameishukuru sana Benki ya CRDB, na kuahidi kuwa yale waliyoyakusudia
kuyafanya yatafanyika kwa kiwango kikubwa sana na habari zitawafikia
watu wengi tofauti na hapo awali.
No comments:
Post a Comment