Waziri
wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi , Profesa Adolf Mkenda(Mb)
ameipongeza Benki ya NMB kwa kuwa mstari wa mbele kuinua Sekta ya Elimu
nchini kwa kutoa mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu wanaotoka kwenye
familia zenye uhitaji.
Profesa Mkenda aliishukuru NMB wakati
akiwakilisha Bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi
kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Aidha, alibainisha kuwa, Serikali
inaendelea kutafuta vyanzo mbalimbali vya kugharamia Elimu ya Juu nchini
kwa lengo la kuongeza fursa za upatikanaji wa Elimu ya Juu, ili
kuendana na mahitaji yanayotokana na ongezeko kubwa la uhitaji wa mikopo
kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu.
Benki ya NMB imetenga kiasi cha
Shilingi Bilioni 200 kwa kuanzia katika mwaka wa fedha 2022/23 kwa ajili
ya kuanza kutoa mikopo ya elimu. Fedha hizo zitatolewa kwa utaratibu
maalum wa kibenki na kwa mujibu wa makubaliano rasmi kati ya Wizara na
NMB.
Mikopo hiyo itaongozwa na masharti yafuatayo:
· Itatolewa kwa riba nafuu.
· Itatolewa kuanzia ngazi ya stashahada (Diploma) na masomo ya Umahiri (Postgraduate).
· Itatolewa kwa waajiriwa wanaotaka kujiendeleza kielimu.
Katika
hili, NMB itasaidia kupunguza idadi ya waajiriwa wanaowaombea watoto
wao mikopo kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu na hivyo kutoa fursa
zaidi kwa waombaji wenye uhitaji.
Hivi karibuni, benki ya NMB
ilizindua ‘Nuru Yangu Scholarship and Mentorship Program’ kwa ajili ya
kusaidia elimu nchini, kwa lengo la kukata mnyororo wa umasikini na
kuendeleza kizazi kijacho cha viongozi, kwa kutumia njia ya kuongeza
idadi ya wanafunzi wanaojiunga na sekondari (A-Level) na Elimu ya Juu.
Kupitia
program hiyo, wanafunzi watalipiwa kila kitu ikiwemo ada, fedha za
kujikimu, fedha za mafunzo kwa vitendo, bima ya Afya na Kompyuta
mpakato. `
Waziri
wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Adolf Mkenda (Mb)
akizungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi Ruth Zaipuna
katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, baada ya uwasilishaji wa Bajeti
wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa fedha 2022/2023.
No comments:
Post a Comment