Katika
kuhakikisha afya za Watanzania zinakuwa salama na bora, Benki ya NMB
imeshirikiana na kampuni ya bima ya Jubilee kukuleta bima ya afya ili
kumkinga mteja dhidi ya magonjwa au ajali itakapotokea.
Kuna vifurushi viwili kwenye bima hii;
Bima
ndogo (J-Afya) ambayo inamkinga mteja kwa ajili ya matibabu ya kutwa na
kulazwa. Katika kifurushi hiki, Bima itagharamia mwanachama na familia
yake kwa mwaka, Milioni 6 kwa matibabu ya kulazwa, na Milioni 1.2 ya
kutwa.
Mtoto pekee yake atagharamiwa kwa Sh.Milioni 3. Kutakuwa
na gharama za ziada endapo mwanachama atahitaji huduma zaidi ya
zilizoainishwa kwenye mpango wake wa bima.
Aidha, Bima kubwa
(J-care) imegawanyika katika makundi manne; Royal, Executive, Advanced
na Premier, na malipo ya kila mwaka (premium) yatategemea na ukubwa wa
familia pamoja na Umri wa mwanachama na mwenza wake.
Faida ya
bima hii ni kupata matibabu ya kutwa na kulazwa, matibabu ya meno na
macho, mkono wa pole endapo mwanachama atafariki, uzazi na vipimo
vikubwa kama MRI.
Bima ya J-care inakupa huduma bora za matibabu
kwa urahisi katika hospitali zilizoko kwenye mpango wa bima
zinazopatikana nchi nzima.
Pata bima yako kupitia *150*68# au
kupiga simu nambari 0800 002 002 bure Kabisa, barua pepe
Bancassurance@nmbbank.co.tz au fika tawi la NMB lililopo karibu yako.
Umebima?- SiNgumuKihivyo!
No comments:
Post a Comment