AfisaMtendaji
Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, akipiga makofi wakati maofisa wa
ngazi za juu wa benki hiyo waliposhika mabango kuashiria uzinduzi wa
Hati Fungani Maalum ‘NMB Jasiri Bond’ uliofanyika leo Februari 7, 2022
jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Idara ya Wateja
Binafsi, Aikansia Muro, Afisa Mkuu wateja Binafsi na Biashara, Filbert
Mponzi, Afisa Mkuu Hazina, Azizi Chacha na Afisa Mkuu Huduma Shirikishi,
Nenyuata Mejooli.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, akizungumza wakati wa
uzinduzi wa Hati Fungani Maalum ‘NMB Jasiri Bond’ uliofanyika leo
Februari 7, 2022 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Mkuu Wateja
Binafsi NMB, Filbert Mponzi na Afisa Mkuu Hazina, Azizi Chacha.
……………………………………
Benki
ya NMB imetangaza kuanza kuuzwa rasmi kwa hati fungani ya miaka mitatu
inayomlenga mwekezaji yeyote aliye tayari kuwekeza katika taasisi hiyo
kwa ajili ya kupata riba nzuri.
Kiwango cha chini cha uwekezaji
kwenye hati fungani hii ni TZS 500,000 na itaweza kununuliwa kutoka
kwenye tawi lolote la Benki ya NMB au kwa madalali wa hisa waliosajiliwa
na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).
Hati fungani
hii ya NMB Jasiri inategemea kukusanya kiasi cha Shilingi bilioni 25
kupitia mauzo ya dhamana hii, lakini ikiwa na kipengele cha kuongeza TZS
bilioni 15 zaidi. Mapato ya Hati fungani hii ya NMB Jasiri yatatumika
kusaidia utoaji wa mikopo kwa biashara na makampuni yanayomilikiwa au
kusimamiwa na wanawake pamoja na biashara ambazo bidhaa na ama huduma
zake zinamnufaisha mwanamke.
Hii ni hati fungani ya kipekee na
ya kwanza kutolewa kwenye ukanda wa Afrika Mashariki mahsusi kwa ajili
ya kuwawezesha wanawake kijamii na kiuchumi na inaendelea kuonyesha tu
jinsi Benki ya NMB inavyoendelea kuunga mkono juhudi za kufikia Malengo
Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs), hasa lengo endelevu namba 5 (SDG 5)
linalohusu Usawa wa Kijinsia na lile la namba 10 (SDG 10) lililojikita
katika kupunguza tofauti za kijinsia.
Wawekezaji kwenye hati
fungani hii watapata riba ya asilimia 8.5 kwa mwaka itakayolipwa kila
robo mwaka wakati wa kipindi chote cha miaka mitatu mpaka mwezi Machi
mwaka 2025. Riba itakayolipwa itakatwa kodi ya zuio.
Aina hii ya
hati fungani pia hutoa fursa kwa wawekezaji wadogo kuwekeza katika
dhamana za (viwango vidogo) kiasi kidogo, kupanua wigo wa uwekezaji na
kushiriki katika soko la hati fungani hivyo kuongeza ushirikishwaji
kifedha na ufikiaji huduma unaostahili kwa kutumia mtandao wa benki yetu
unaopatikana kirahisi.
Uuzaji wa Hati Fungani ya NMB Jasiri
utaanza leo Februari 7, 2022, hadi Machi 21, 2022. Maombi yote ya
kuinunua Hati fungani hii yatapita kwenye matawi yote 226 ya NMB au kwa
madalali waliosajiliwa na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).
Karibuni tuwekeze!
No comments:
Post a Comment