Na Amiri Kilagalila,Njombe
Mvua
iliyonyesha siku mbili mfululizo imebomoa madaraja matatu wilayani
Ludewa mkoa wa Njombe na kusababisha shughuli za usafirishaji kutoka
Ludewa kwenda maeneo mbali mbali kusimama
Madaraja yaliyobomolewa
ni Nyapinda njia panda ya kwenda Ibumi,daraja la Muhoro,daraja la chuma
la Mhambalasi linalounganisha kata ya Mkomang'ombe na Ibumi pamoja
daraja la Ludewa mjini kwenda Ludewa vijijini.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo kwa njia ya simu mkuu wa wilaya ya Ludewa Andrea
Tsere,amesema mvua hizo zimenyesha usiku febuari 22 na 23 mwaka huu.
Mkuu
wa wilaya amewataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali ikiendelea
kufanya jitihada za haraka kuweza madaraja ya muda na kuanza kuanza
ujenzi wa kujenga madaraja ya kudumu.
Aidha mkuu wa wilaya
amesema tayari amefanya mawasiliano na wakala wa barabara Tanroad mkoa
wa Njombe ili kuhakikisha hatua za haraka zinachukuliwa ili kunusuru
maisha ya watoto wa shule pamoja na wananchi maeneo hayo.
No comments:
Post a Comment