Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
SERIKALI
iko mbioni kuwaondolea karaha ya Ukosefu wa huduma ya usafiri wa mabasi
ya haraka kwa wakazi wa Mbagala jijini Dar es Salaam ,ifikapo Mwezi
Machi 2023 ,ambapo kwasasa mkandarasi wa ujenzi wa miundombinu amefikia
asilimia 44.4 .
Aidha Wakala wa mabasi yaendayo haraka (DART ) unakwenda kuboresha miundombinu na Mazingira ya utoaji huduma kwa Kibaha na maeneo mengine ambayo mabasi hayo yameanza kutoa huduma.
Akizungumza
na waandishi wa habari mjini Kibaha baada ya kumaliza mafunzo ya wiki
Saba ,kupitia wizara ya uwekezaji, viwanda na biashara chini ya Taasisi
zilizo chini yake Chuo cha elimu ya biashara (CBE ) na SIDO pamoja na
kitengo Cha KAIZEN , Mtendaji Mkuu wa wakala wa Mabasi yaendayo haraka
(DART)Dkt.Edwin Mhede alieleza, wakati wakitarajia ujenzi kukamilika,
Mkandarasi atakapokabidhi na DART watakabidhi kwa mtoa huduma wa mabasi .
Dkt.Mhede
alieleza, ujenzi huo ni ushirikiano wa Taasisi tatu ambapo Wakala wa
barabara TANROADS wakiwa ni wasimamizi wa ujenzi wa miundombinu,UDART na
Wizara mbili ya ofisi ya TAMISEMI na ujenzi ambao ni wasimamizi wa
mradi.
"Licha ya
mafanikio na changamoto ambavyo vilikuwa vinaonekana kwenye sekta yetu
ya usafirishaji Wizara ya Uwekezaji ,Viwanda na biashara chini na
Taasisi ya CBE, SIDO na kitengo chake cha KAIZEN imeona itushirikishe
DART ione iliyofanya kwenye viwanda kama yanaweza kuleta tija na kwenye
sekta yetu:"
:"Katika
mafunzo tuliyoyapata tunahitaji kuwa na mabadiliko ya kifikra baina yetu
DART na UDART tumekubaliana kufanya maboresho kwenye huduma zetu
kuondoa karaha kwa wateja wetu wakiwemo wa ruti za Kibaha na maeneo
mengine" alisema Dkt.Mhede.
"Tunakiri
bado kuna uhitaji mkubwa wa mabasi kwa mkoa wa Dar es Salam peke yake
japo ina magari mengi binafsi lakini inatoa asilimia 10 pekee ya
mahitaji ya usafiri na asilimia 90 wanategemea usafiri wa umma" alisema
Dkt Mhede.
Msimamizi wa
Kitengo cha KAIZEN kutoka Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Jane
Lyatuu alisema mafunzo yametolewa kwa wiki Saba na yatakuwa endelevu.
Meneja
upangaji ratiba na udhibiti kutoka kampuni ya mabasi yaendayo kasi
UDART Daniel Madili alibainisha, kupitia mafunzo hayo wanakwenda kufanya
maboresho kwenye huduma zao kwa wananchi.
Baadhi
ya wakazi Kibaha , Loliondo akiwemo Josephine Dachi na Joseph Gabriel
waliipongeza Serikali kwa kuwasogezea huduma ya mwendokasi hadi Kibaha.
No comments:
Post a Comment